Meneja Miradi na Biashara wa DSE, Patrick Mususa.
Na Ally Daud – MAELEZO, Dar Es Salaam
IDADI
ya mauzo katika soko la hisa la Dar es salaam (DSE) imeshuka kwa
asilimia 78 kutoka Tsh. Bilioni 29.8 hadi Tsh. Bilioni 6.4 kwa kipindi
cha wiki moja iliyopita.
Aidha
idadi ya hisa zilizouzwa katika soko hilo pia zimeshuka kwa asilimia
60 kutoka Tsh. Milioni11.2 hadi kufikia Tsh. Milioni 4.3 kutokana na
makampuni mengi kutowekeza katika soko la hisa.
Akizungumza
na waaandishi wa habari leo (Jumatatu Septemba 07, 2015) Meneja Miradi
na Biashara wa DSE, Patrick Mususa alisema kuwa hata hivyo idadi ya
mtaji katika soko umekuwa kutoka tilioni 21.8 hadi tilioni 21.9 ikiwa ni
pamoja na ongezeko la idadi ya mtaji wa makampuni ya ndani kutoka Tsh.
Trilioni 9.7 hadi Tsh. Trilioni 9.9.
Aidha
Bw.Mususa ameitaja benki ya CRDB kuwa ndiyo inayoongoza kuuza hisa zake
katika soko hilo ikiwa na asilimia 91, ikifuatiwa na Kampuni ya Bia
Tanzania (TBL) ikiwa na asilimia 7 na Benki ya NMB ikiwa na asilimia
0.5.
Kwa
mujibu wa Mususa alisema kampuni ambazo zinaongoza kwa ongezeko la bei
katika soko la hisa kuwa ni Uchumi Super Market ikiwa na asilimia 5.5
ikifuatiwa na Benki ya KCB ikiwa na asilimia 4.4 pamoja na benki ya NMB
3.5
“Viashiria
vya soko katika huduma za kibenki vimeongezeka kwa alama 62, hisa za
benki ya NMB zimeongezeka kwa pointi 3.5 ikifuatiwa na sekta ya viwanda
kwa alama 20 kutokana na ongezeko la bei ya hisa za TBL”
Mususa
alifafanua kuwa pamoja na viashiria vya kibiashara kushuka kwa alama 4
kulikochangiwa na punguzo la bei ya hisa za swissport kwa asilimia 0.13,
kwa ujumla kiashilia cha soko kimeongezeka.
“DSE
tumeboresha huduma zetu kwa kuanzisha huduma ya kimtandao ya DSE
mobile Trading ili kuwawezesha watumiaji wa huduma hizo kujiunga ,
kununua na kuuza hisa kupitia simu ya mkononi kwa kupiga *150*36#”.
No comments:
Post a Comment