Kampuni
ya simu ya Tigo Tanzania itasitisha huduma zake maarufu za kutuma na
kupokea fedha ya Tigo Pesa wikendi hii kwa muda wa saa 17 ili kufanya
maboresho ya huduma hiyo.
Taarifa
iliyotumwa kwa vyombo vya habari na kampuni ya simu jijini Dar es
Salaam inasema kuwa kusitishwa kwa huduma ya Tigo Pesa kuanzia Jumamosi
usiku hadi Jumapili mchana utakuwa mwendelezo wa zoezi la uboreshaji wa
huduma za kifedha za simu kwa takribani siku saba, “ kuifanya huduma ya
Tigo Pesa kuwa ya kasi, imara na rahisi kupatikana.”
Huduma
za Tigo Pesa zitakazo athirika kutokana na zoezi la marekebisho ni
pamoja na ubadilishaji wa nenol a siri na usajili wa wateja wapya ambazo
hazitakuwepo kuanzia Septemba 8 hadi 15, ubadilishaji namba ya simu
kuanzia Septemba 12 hadi 15 na uboreshaji wa simu utakosekana kuanzia
Septemba 6 hadi 16
“Tunaomba
radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza katika kipindi chote
tutakapokuwa tukipambana kukuboreshea huduma yako ya Tigo Pesa kuwa ya
kasi, imara na upatikanaji rahisi,” ilisema sehemu ya habari hio.
Taarifa inayofanana na hii imechapishwa kwenye vyombo vya habari pamoja
na kwenye mitandao ya kijamii.
Tigo
Pesa ni huduma maarufu ya kifedha kwa njia ya simu za mkononi nchini
Tanzania ikiwa na zaidi ya wateja zaidi ya milioni 4 kote nchini.Huduma
zinazotolewa na Tigo Pesa ni pamoja na ubadilishanaji wa fedha kati ya
wateja wanaotumia mtandao wa Tigo na kati ya wale watumiao mitandao
mingine, pia uhamishaji wa pesa kutoka kwenye simu kwenda Benki na
kutoka Benki kwenda kwenye simu.
Mwaka
uliopita Tigo Pesa ilikuwa huduma ya kwanza ya kifedha kwa njia ya simu
duniani kwa kuvuka mipaka na kuwezesha uhamishaji wa fedha
iliyobadilishwa kwenda Rwanda na pia kuwa huduma ya kwanza ya kifedha
kwa njia ya simu duniani kwa kutoa gawio la faida kwa wateja wake
kulingana na kiasi cha fedha walichokihifadhi kwenye mfuko wao wa Tigo
Pesa.
No comments:
Post a Comment