Habre amekataa kuitambua mahakama hiyo
Kesi ya
uhalifu wa kivita dhidi ya kiongozi wa zamani wa Chad Hissene Habre
inaendelea hii leo katika mji mkuu wa Senegal Dakar licha ya kiongozi
huyo kukataa kuitambua mahakama hiyo.
Bwana Habre alilazimishwa kuingizwa mahakamani kwa nguvu alipokataa kuingia mwenyewe.
Kiongozi
huyo alishikwa na walinzi alipomfokea hakimu pale upande wa mashtaka
ulipoanza kusoma orodha ya majina ya watu waliouawa ama kupotea wakati
wa utawala wake.
Bwana Habre anatuhumiwa kwa kuamrisha mauaji ya watu 40,000 wakati wa utawala wake mnamo miaka ya 80.
Habre alilazimishwa kuingizwa mahakamani kwa nguvu
Pia anakabiliwa na mashtaka ya mateso na uhalifu dhidi ya ubinadamu. BBC
Kesi hiyo
ilihairishwa mwezi Julai baada ya bwana Habre kupinga mahakama hiyo
akiitaja kuwa isiyo halali ambapo pia aliwashauri mawakili wake
wasihudhurie.
Mahakama baadaye ilimpa mawakili ambao waliomba takriban siku 45 iliwajifahamishe yanayojiri katika kesi hiyo.
Siku 45
baadaye mawakili watatu walioteuliwa wamepata muda wa kutosha kuiangalia
kesi hiyo lakini mteja wao hawatambui na amekataa kuwasiliana nao.
Jaji wa mahakama ya Burkinabe, Gberdao Gustave Kam ataamua iwapo kesi hiyo itaendelea bila upande wa utetezi wa Hissene Habre.
Tangu
mwanzo wa utaratibu wa kesi hiyo, Hissene Habre, mwenye umri wa miaka
72, amekuwa akikataa kutambua uhalali wa mahakama maalum ya Afrika,
ambayo iliundwa na Umoja wa Afrika mwaka 2013, ili kushugulikia kesi
yake nchini Senegal.
Rais huyo wa zamani wa Chad hajawahi kujibu maswali ya jaji.
Habre anatuhumiwa kwa kuamrisha mauaji ya watu 40,000
Afisa wa
Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch, Reed Brody
amesema kwa kukataa kushirikiana na mahakama, Habre anajaribu
kuchelewesha utaratibu wa mahakama, ambayo ina bajeti ya dola milioni
9.5.
Kucheleweshwa kwa kesi hiyo kwa siku 45 kutaongeza bajeti kwa asilimia tisini.
Kesi hiyo ilikadiriwa kuchukua muda wa siku 90 pekee.
Waathirika ambao walifanya kampeni ya miaka 25 kuhakikisha ameshtakiwa wanatarajia kuwa mahakama hiyo itatenda haki.
Rais huyo wa zamani wa Chad hajawahi kujibu maswali ya jaji
Hii ni
mara ya kwanza rais wa nchi kushtakiwa katika nchi nyingine ya Afrika
kwa shutma za unyanyasaji, uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya
binadamu.
Mwendesha
mashtaka wa mahakama hiyo maalum atajaribu kuwasilisha ushahidi
kuonyesha kuwa Habre aliamuru mauaji na unyanyasaji wa maelfu ya watu
waliompinga kisiasa.
Tume ya
ukweli iliyoundwa kuchunguza madai hayo ilipata ushahidi wa mauaji ya
takriban watu 4,000 na ikakadiria kuwa huenda idadi hiyo ikawa mara 10
zaidi.
No comments:
Post a Comment