Wayahudi waandamana dhidi ya wanamgambo - LEKULE

Breaking

2 Aug 2015

Wayahudi waandamana dhidi ya wanamgambo

Maelfu ya watu nchini Israeli wameshiriki kwenye maandamano wakiitaka serikali kuchukua hatua kali zaidi dhidi ya wayahudi wanaotajwa kuwa wanamgambo.

Waandamanaji katika mji wa Tel Aviv walionyesha uzalendo wao kwa familia ya mtoto Mpalestina ambaye aliuawa siku ya ijumaa wakati nyumba katika eneo la ukingo wa magharibi ilipochomwa moto na wayahudi wenye itikadi kali.

Maandamano mengine yalifanyika katika eneo kulikofanyika shambulizi siku ya alhamis ambapo watu sita walidungwa visu wakati wa mkutano wa wapenzi wa jinsia moja.




No comments: