Rais Kikwete aifariji familia ya marehemu mzee Peter Kisumo - LEKULE

Breaking

6 Aug 2015

Rais Kikwete aifariji familia ya marehemu mzee Peter Kisumo

jk1
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini kwenye kitabu cha maombolezo Upanga jijini Dar es salaam alipokwenda kwenye msiba wa mmoja wa wanasiasa wakongwe nchini, Marehemu Mzee Peter Kisumo,  aliyefariki dunia Jumatatu katika Hospitali ya taifa ya Muhimbili ambako alikuwa anapatiwa matibabu ya Figo. Marehemu Mzee Kisumo alipata kuwa Mzee wa Chama cha TANU, Muasisi na mdhamini wa Chama cha CCM na aliyeshikilia nafasi nyingi za uongozi ndani ya Serikali na utumishi wa umma ukiwemo uwaziri.
jk2

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji mjane wa wanasiasa  wakongwe nchini, Marehemu Mzee Peter Kisumo,  aliyefariki dunia Jumatatu katika Hospitali ya taifa ya Muhimbili ambako alikuwa anapatiwa matibabu ya Figo. Marehemu Mzee Kisumo alipata kuwa Mzee wa Chama cha TANU, Muasisi na mdhamini wa Chama cha CCM na aliyeshikilia nafasi nyingi za uongozi ndani ya Serikali na utumishi wa umma ukiwemo uwaziri.
(Picha na IKULU).



No comments: