Mdosi amfanyia mbaya… - LEKULE

Breaking

25 Jul 2015

Mdosi amfanyia mbaya…

Mdosi mmoja ambaye ni bosi wa kampuni moja ya kusafirisha mafuta jijini Dar aliyefahamika kwa jina la Jetti anasakwa na polisi kwa RB; CHA/RB/5871/2015 SHAMBULIO LA MWILI akidaiwa kumfanyia kitu mbaya deveva wake aitwaye Deogratius.
Tukio hilo la kusikitisha linadaiwa kutokea Julai 18, mwaka huu maeneo ya Mbagala Mission jijini Dar ambapo dereva huyo alipigwa, akajeruhiwa ikiwa ni pamoja na kung’olewa meno kabla kukoswakoswa risasi.
Chanzo ni nini?
Akisimulia mkasa huyo, Deogratius alidai: “Siku ya tukio nilikuwa natokea Kongo nikiwa nimeongozana na gari nyingine ya kampuni. Kwa kuwa nilikuwa na usingizi, nilipofika Iringa nilipumzika lakini mwenzangu akaendelea na safari. Asubuhi nikaondoka.
“Nilipofika Mikumi (Morogoro) nililiona lile gari la mwenzangu limeanguka, nikasimama na kwenda kuangalia lakini sikuona mtu, nikapiga simu ofisini kuwajulisha lakini bosi mmoja akaniambia wanazo taarifa, mimi nirudi tu ofisini.
“Nilipofika ofisini usiku saa moja nikashangaa bosi wangu mmoja anakuja na kunishika kwa staili ya ‘Tanganyika jeki’ huku yule bosi wangu Mhindi akinipiga ngumi, mateke na kitako cha bastola.
“Damu zilinitoka sana, nilipouliza kwa nini napigwa wakadai kuwa eti mimi nimemtorosha dereva mwenzangu yule aliyepata ajali Mikumi, jambo ambalo niliwakatalia.
“Bosi akachomoa bastola na kufyatua risasi hewani, nilipoona vile nikaanza kukimbia ndipo aliponifyatulia mbili lakini zilinikosa, moja ikapiga kwenye kioo cha ofisi yake.
“Walinikimbiza na kunikamata kisha wakaendelea kunipiga hadi usiku walipokuja wafanyakazi wengine na virungu, kwa kipigo kile nilipoteza fahamu.
“Niliposhituka nikajikuta kwenye gari lenye vioo ‘tinted’, niligundua tupo mitaa ya Upanga. Nikapata akili ya kuchukua simu yangu na kuwasiliana na ndugu zangu ambapo wakati nikifanya hivyo, wale watu waligeuza gari na kunirudisha Kituo cha Polisi Chang’ombe.
“Kufika pale wakatoa maelezo yao na kwa kuwa ndugu zangu walishafika pale, wakanisaidia kupata fomu ya matibabu kutoka polisi ‘PF3’, nikaenda kutibiwa.
“Julai 19 ndipo wakaja viongozi wa Chama cha Madereva wa Malori Tanzania (CHAMAMATA) na kunichukua tena mpaka Kituo cha Polisi cha Chang’ombe ambapo niliandikisha maelezo na kupewa RB; CHA/RB/5871/2015 SHAMBULIO LA MWILI,” alieleza Deogratius kwa masikitiko.
Akaelezwa kuwa upelelezi kuhusiana na tukio hilo unaendelea na tayari watuhumiwa wawili wamekamatwa ila bosi aliyekuwa kimbelembele (Mdosi) na wengine hawajakamatwa.

Waandishi wetu walifanya jitihada za kumpata bosi huyo Mdosi ambapo alipopigiwa simu alizuga kisha akatoa namba ya simu ya mtu mwingine na kutaka apigiwe huyo kwani ndiye mwenye ufafanuzi. Naye alipopigiwa hakutoa ushirikiano.


No comments: