DAVIDO NDANI YA NGOMA MOJA NA RIHANNA - LEKULE

Breaking

15 Jul 2015

DAVIDO NDANI YA NGOMA MOJA NA RIHANNA

Staa wa muziki kutoka Nigeria, David Adedeji Adeleke ‘Davido’.
Lagos, Nigeria
STAA wa muziki kutoka Nigeria, David Adedeji Adeleke ‘Davido’amefungukia ujio wake mpya kupitia mitandao ya kijamii kuwa yupo mbioni kufanya kolabo na Rihanna.
Rihanna.
Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Davido aliulizwa na mashabiki baada ya kufanya kolabo la kimataifa na rapa kutoka Marekani, Meek Mill kupitia Ngoma ya Fans Mi, mashabiki watarajie nini ndipo alisema yupo mbioni kutoa ngoma na Rihanna lakini hakuweka wazi mipango kamili inayoendelea.

Davido kwa sasa ni mmoja wa wasanii kutoka Afrika, anayewakilisha Nigeria kwenye Tuzo za MTV Africa (MAMA) akiwania vipengele vitatu sambamba na staa kutoka Tanzania, Diamond Platnumz.

No comments: