Mwili wa Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti Alhaj Sheikh Shaban Issa Bin Simba Kusafirishwa Kesho Kwenda Mkoani Shinyanga Kwa Taratibu za Mazishi - LEKULE

Breaking

16 Jun 2015

Mwili wa Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti Alhaj Sheikh Shaban Issa Bin Simba Kusafirishwa Kesho Kwenda Mkoani Shinyanga Kwa Taratibu za Mazishi

MWILI wa  Mufti ,Alhaj Sheikh Shaban Issa Bin Simba unataraji kusafirishwa kesho Jumanne Juni 16, kuelekea mkoani Shinyanga kwa ajili ya taratibu za mazishi.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye Makao Makuu ya Baraza Kuu la Waislam Tanzania (Bakwata), Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaj  Mussa Salum, amesema mwili wa marehemu utaswaliwa kesho katika Msikiti wa Msilimu, viongozi mbalimbali wa dini na serikali watakuwepo.

Amesema marehemu amefikwa na umauti huo, baada ya kusumbuliwa sana na sukari,Shinikizo la Damu (BP)  pamoja na Figo.

Hata hivyo amesema kuwa jana (Jumapili) Mufti alifanyiwa oparesheni ya figo katika Hospitali ya TMJ Jijini Dar es Salaam.


Salum amesema marehem anatarajiwa kuzikwa Alhamis mkoani mkoani Shinyanga .

No comments: