Dar es Salaam.
Balozi Amina Salum Ali amesema Rais wa Zanzibar anayemaliza muda wake, Dk Ali Mohamed Shein bado anastahili kupewa nafasi ya kuongoza Wazanzibari.
Balozi Amina Salum Ali amesema Rais wa Zanzibar anayemaliza muda wake, Dk Ali Mohamed Shein bado anastahili kupewa nafasi ya kuongoza Wazanzibari.
Balozi
Amina ambaye ni Balozi wa Kudumu wa Umoja wa Afrika (AU) nchini
Marekani alitoa kauli hiyo jana katika Kipindi cha Funguka’, kilichoanza
kurushwa na Azam TV, baada ya kuulizwa swali na mwendeshaji wa kipindi,
Tido Mhando.
Mwanadiplomasia huyo alitoa jibu hilo
alipoulizwa kwa nini hakutaka kugombea tena urais wa Zanzibar wakati
alionyesha nia ya kuongoza Zanzibar mwaka 2000.
Akijibu
swali hilo alisema, “Kwa sasa tunapita kwenye kipindi kigumu na mie
ninakiri kwamba, Rais tuliyenaye anajitahidi, kwa sababu Serikali ya
Umoja wa Kitaifa (SUK) ni mpya, hajamaliza muda wake na tunaona jinsi
alivyoongoza,” alisema.
Alisema ni vyema Dk Shein akapewa nafasi ya kuendelea kuongoza licha ya kuwapo kwa wanachama wanaotamani nafasi hiyo.
Mwombaji huyo wa urais wa muungano kupitia CCM alisema Wazanzibari wengi wameonyesha nia ya kumwamini Dk Shein.
Kuhusu
SUK na hali ya kutofautiana kisiasa, Balozi Ali alisema umoja huo
ulikuwa ni majaribio ambao umeonyesha unafuu mkubwa katika mahusiano ya
Wazanzibari, hivyo serikali hiyo haitakiwi kuvunjwa.
Kuhusu Muungano
Akizungumzia
mahusiano ya muungano kati ya Tanzania Bara na Zanzibar, Balozi Ali
alisema changamoto kubwa iliyopo ni kukosekana kwa utekelezaji wa mambo
yanayojadiliwa ndani ya vikao vya serikali hizo mbili.
“Mambo
yalijadiliwa na kukubaliwa lakini kila jambo lilionekana kama ni nyeti
au la kisiasa au haliwezekani, matokeo yake mambo yamekuwa ni mengi
mpaka kufikia hatua ya kufanyia mapitio ya katiba,” alisema na kuongeza:
“Mambo
yanayowaumiza Zanzibar ni masuala ya uchumi na upande mwingine ni
masuala ya kisiasa na Itifaki. Ilikuwa wakati mwafaka wa kuyafanyia
maboresho, ukiangalia katika mapendekezo ya Katiba kama kuna mambo
ambayo yangefanyiwa kazi, yangeweza kuleta nafuu katika mfumo wetu,”
alisema.
Alipoulizwa ni kwa jinsi gani ataondoa kero na
changamoto za muungano huo, mgombea huyo alisema Muungano huo haukuwa
na kero ila zilikuwa changamoto tu ambazo zimebadilika kuwa kero baada
ya kuchukua muda mrefu bila kushughulikia.
Alisema;
“Kwa mfano suala la Benki Kuu au ugawanaji wa mapato, pia tulikubaliana
kuwa na ufumbuzi wa muda katika ugawanaji mapato, lakini kama ni hiyo
pia kulikuwa na tume ya pamoja ya fedha ndani ya Katiba lakini
haikuanzishwa.
“Sasa kama kuna jambo ambalo hamlimalizi
leo, litakuwa kero tu..sasa mimi sijaona kero hapo ila kwa kuwa
serikali zetu mbili tumeshindwa kutatua, nia ya dhati ya kuondoa kero
hizo lazima ionekane kwa vitendo.
Serikali yake
Akizungumzia
aina ya serikali yake atakayoitumia baada ya kupewa ridhaa na
Watanzania kupitia CCM, alisema kipaumbele chake ni kufufua viwanda vya
ndani ili kuongeza kipato cha Watanzania.
Pia alisema rushwa, ubadhirifu, ufisadi, mikataba mibovu na kutojali wananchi ni mambo ambayo yameendelea kuwaumiza Watanzania.
Alipoulizwa
juu ya mazingira ya kuogopana kwa viongozi katika kuwashughulikia
mafisadi, Balozi Ali alisema utaratibu uliopo ufanyiwe marekebisho ili
wahusika washughulikiwe.
Alisema ni muhimu kuweka mahakama maalumu na mtuhumiwa kusimamishwa kwa muda.
“Kesi
siyo isichukue miaka sita, pia uwajibikaji siyo majadiliano, inapotokea
lazima waziri awajibike mara moja, unapokuwa rais na chama chako
unapewa dhamana tu na inapotokea kosa lazima uwajibike kisiasa,lakini
naona imekuwa tatizo mpaka mtu aondolewe na rais, hapana.” alisema na
kuongeza:
Kuhusu hali ya kujitokeza kwa wingi wagombea
urais, Amina alisema; “ Siyo tatizo ila urais si jambo la majaribio,
tuwaachie Watanzania wachague mwenye sifa, aliyekuwa bora, mwenye uwezo
na mimi ninazo sifa zote na ninaamini kuwa bora zaidi kuliko wote.”
No comments:
Post a Comment