Saudia haina haki kuzuia misaada yaYemen - LEKULE

Breaking

16 May 2015

Saudia haina haki kuzuia misaada yaYemen

Saudi Arabia haina haki ya kuchukua maamuzi kuhusu misaada ya kibinadamu inayoelekea Yemen nchi ambayo inakabiliwa na hujuma ya kijeshi ya watawala wa Riyadh.
Hayo yamesemwa na naibu waziri wa mambo ya nje ya Iran Hossein Amir-Abdollahian anayeshughulikia masuala ya Kiarabu na Kiafrika.
Ameongeza kuwa hatua ya utawala wa Saudia kuzuia misaada ya kibinadamu Yemen imepelekea watu katika mikoa 20 nchini humo kukosoa mahitajio ya dharura. Amir-Abdollahian ameongeza kuwa Iran iko tayari kutuma misaada  katika maeneo yote ya Yemen. Tayari Saudia imeshazuia ndege kadhaa za Iran zifikishe misaada  ya chakula na dawa nchini Yemen. Hivi sasa meli ya misaada ya Iran inayosheheni chakula na dawa iko njiani ikielekea Yemen. Iran imeionya Marekani na Saudia  kuwa hujuma yoyote ya kijeshi dhidi ya meli hiyo itaibua moto katika eneo. Ikumbukwe kuwa Saudia ilianzisha hujuma dhidi ya Yemen mnamo Machi 26 bila ya idhini ya Umoja wa Mataifa. Lengo la hujuma hiyo ni kuiangusha harakati ya Ansarullah iliyoko madarakani na kumrejesha rais wa zamani wa nchi hiyo Abd Rabbuh Mansur Hadi ambaye ni kibaraka wa Saudia.

No comments: