Wayne Rooney aomba radhi - LEKULE

Breaking

18 Feb 2015

Wayne Rooney aomba radhi



Golikipa wa timu ya Preston Thorsten Stuckmann ameeleza kuwa mshambuliaji Wayne Rooney

alimuomba msamaha baada ya kuanguka katika eneo la hatari na kupata mkwaju wa penati.

Kipa huyu alimwangusha Rooney wakati mchezaji huyo akielekea kufunga bao na kusababisha penati,

Stuckmann, alisema "Rooney aliniomba msamahani na kuniambia ilikua ni nafasi yake ya kupata penati".

"Naamini tukio kama lile lingetokea kwenye goli la Manchester United toka kwa mshambuliaji wetu refa asingeweza kutupa penati sina shaka na hilo".

"Sisemi kama haikuwa penati, nachokisema hakukua na mgongano wowote"

Rooney alifunga mkwaju huo wa penati na kuipa timu yake ushindi mnono wa mabo 3-1dhidi ya Preston.

No comments: