Kigwangalla Awapa Pole CHADEMA Kwa Kumchagua Dr. Machinji Kuwa Katibu Mkuu Wao - LEKULE

Breaking

14 Mar 2016

Kigwangalla Awapa Pole CHADEMA Kwa Kumchagua Dr. Machinji Kuwa Katibu Mkuu Wao


Zikiwa zimepita siku mbili toka kupatikana kwa Katibu Mkuu mpya wa CHADEMA Dk Vincent Mashinji,  Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Hamisi Kigwangalla  ameibuka na kuwapa pole CHADEMA kama walimchagua Katibu Mkuu wao kwa kuangalia historia yake.
 
Kupitia Account yake ya Facebook Dk Hamisi Kigwangalla anakiri wazi kuwa Dkt. Mashinji ni msomi mzuri na mwanasiasa mzuri ingawa anadai hana uhakika kama alimaliza masomo ya ubingwa.
 
"Ndg., Dkt. Mashinji is a friend, brother and colleague. Hakuwahi kutuokoa mimi na Dkt. Ulimboka, na hakuwahi kuongoza mgomo, sema alishiriki mgomo ulioongozwa na mimi na Dkt. Ulimboka. 
"Kiukweli, ni mwanasiasa mzuri, msemaji, msomi mzuri (tumesoma naye MBA chuo kimoja), sina hakika kama alimaliza masomo ya Ubingwa maana alinyanyaswa na Supervisor wake, akasusa akaamua kujiiunga masomo ya MBA na sina hakika sana kuhusu 'msimamo usiotetereka'. 

"Maana baada ya vitisho vya 2005, aliyumba sana na tulimtenga na ku-aVoiD kumualika vikao vya CC ya mgomo. Hivyo, kama kigeZo kilikuwa ni hii historia, pole kwa CHADEMA." Ameandika Dk Kigwangalla

No comments: