MASHINDANO YA NGUMI YA TAIFA YAMALIZIKA TANGANYIKA PACKERS - LEKULE

Breaking

13 Feb 2016

MASHINDANO YA NGUMI YA TAIFA YAMALIZIKA TANGANYIKA PACKERS


Rais wa Shilikisho la ngumi za Ridhaa Nchini BFT Mutta Rwakatare katikati akimkabidhi Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi Rajabu Mhamila ‘Super D’ mchango uliotolewa na wadau mbalimbali kwa ajili ya lambilambi ya marehemu Mohamed Chibumbuli kilichotokea juzi Mkoa wa Mtwara Wilaya ya Masasi kushoto ni katibu Mkuu wa shirikisho hilo Makole Mashaga .

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Ndondi Tanzania (BFT), Makore Mashaga kushoto akipeana mkono na kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila ‘Super D’ baada ya kumkabidhi fedha za lambilambi zilizotolewa na wadau mbalimbali wakati wa mashindano ya ngumi ya taifa yaliyofanyika katika viwanja vya Tanganyika Packers Kawe .

Bondia Selemani Kidunda kushoto akimshambulia Mstafa Mtoro wakati wa mashindano ya taifa yaliyomalizika katika viwanja vya Tanganyika Packers Kawe jijini Dar es salaam Kidunda alishinda kwa K.O ya raundi ya kwanza .

Msanii wa filamu, Shamsa Ford  kushoto akipambana na MTANGAZAJI WA TIMES FM, KHADIJA SHAIBU “DIDA’ wakirushiana makonde wakati wa mashindano ya taifa ambapo wao walionesha umwamba. (P.T)


Msanii wa filamu, Shamsa Ford  kushoto  na MTANGAZAJI WA TIMES FM, KHADIJA SHAIBU “DIDA’ wakinyoshwa mikono juu baada ya mpambano wao wakati wa mashindano ya taifa ambapo wao walionesha umwamba

Msanii wa filamu, Shamsa Ford  kushoto  na MTANGAZAJI WA TIMES FM, KHADIJA SHAIBU “DIDA’

Mjumbe wa maendeleo ya wanawake BFT Aisha Voniatis akimvisha medali ya dhaabu bondia Leonard Machichi wakati wa mashindano ya taifa

Mjumbe wa maendeleo ya wanawake BFT Aisha Voniatis akimvisha medali ya dhaabu kwa bondia Zulfa Macho kulia ni bondia Halima Ramadhani wa pili kushoto ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la Ndondi Tanzania (BFT), Makore Mashaga

Bondia Ismail Gaitano kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Mwalami Salum wakati wa mashindano ya taifa yaliyomalizika katika viwanja vya Tanganyika Packers Gaitano alishinda mpambano uho.

No comments: