BLOGU YA WANANCHI YATIMIZA MIAKA MITATU SHEREHE KUFANYIKA LEO HOTELI YA HYATT REGENCY KEMPISKY JIJINI DAR - LEKULE

Breaking

26 Feb 2016

BLOGU YA WANANCHI YATIMIZA MIAKA MITATU SHEREHE KUFANYIKA LEO HOTELI YA HYATT REGENCY KEMPISKY JIJINI DAR


 Mkurugenzi Mkuu wa Blogu ya Wananchi, William Malecela ‘Le Mutuz’ , akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Blogu ya Wananchi, William Malecela ‘Le Mutuz’ , akionesha kompyuta mpakato kwa wanahabari ambayo alianza kuitumia baada ya kuanzisha blogu hiyo miaka mitatu iliyopita.

Mkurugenzi Mkuu wa Blogu ya Wananchi, William Malecela ‘Le Mutuz’ (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kuhusu blogu hiyo kutimiza miaka mitatu na semina itakayowakutanisha wasomi wasio na kazi kuhusu namna ya kujiajiri badala ya kutegemea kuajiriwa.
Na Dotto Mwaibale
KAMPUNI ya Blogu ya Wananchi Media leo itaadhimisha miaka mitatu tangu kuanzishwa kwake, sherehe itakayofanyi Hyatt Regency Kempisky zamani Kilimanjaro jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa blogu hiyo, Wiliam Malecela (Le Mutuz), alisema kuwa wameamua kufanya sherehe kutokana na mafanikio waliyopata katika kipindi hicho, bendi ya muziki wa kizazi kipya ya THT itatumbuiza. 
Alisema licha ya kesho(Leo) kufanya sherehe , leo(Jana) itakuwa na semina maalumu ya vijana 300, ambao watakuwa pamoja na matajiri 6 vijana na vijana watatu viongozi wa wa kitaifa kwa lengo la  kubadilishana mawazo na matajiri na viongozi hao, ambao wataeleza walivyopigana mpaka kufikia walipo kimaisha. 
Alisema alianzisha blogu hiyo baada ya kuisajili kwa msajili wa makampuni (Brela) 2012, ikianza kwa kutembelewa na watu 200 kwa siku lakini kwa sasa inatembelewa na watu 70,000 mpaka 100,000 kwa siku kitu ambacho anajivunia na kuwashukuru wadau.
Kampuni hiyo ilianza kwa mtaji wa dola ya Marekani 500, ikiwa na usajili wa makampuni wa Brela, na inatoa ajira kwa vijana 4 waliomaliza vyuo vikuu nchini na ina ofisi yake katika jengo la Tancot House Sokoine Drive, Dar es Salaam. 
Alisema katika miaka mitatu blogu imeweza kuwa na domain yake wenyewe ya www.williammalecela.com na kuingia kwenye Facebook, Twitter, na Instagram ambapo sasa inarushahabari sehemu mbalimbali kwa wakati mmoja na kuweza kuwafikia watu hadi 500,000 kwa siku.
Alisema mipango ya baadaye ni kuwekeza kwenye kampuni mpya ya  African Swahili Media Radio & Television ambayo tayari imeshapata leseni ya kufungua radio na televisheni ambayo inatazamiwa kuwa hewani  Aprili mwaka huu, kituo cha radio kitakuwa Morogoro na  televisheni Dar es Salaam, anatarajia kutoa ajira zaidi angalau kwa vijana 10.

(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712-727062

No comments: