WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI AKUTANA NA MABALOZI WA MISRI NA DENMARK. - LEKULE

Breaking

13 Jan 2016

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI AKUTANA NA MABALOZI WA MISRI NA DENMARK.

WAZIRI wa Maji, Mhe. Inj. Gerson Lwenge leo amekutana na mabalozi wa Misri na Denmark kwa nyakati tofauti ofisini kwake, Makao Makuu ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Ubungo Maji.

Huu ni mwendelezo wa mazungumzo ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhe. Inj. Lwenge na washirika wa maendeleo na wadau wa Sekta ya Maji ya kuweka mikakati ya kuinua na kuendeleza Sekta ya Maji nchini, mara baada ya juzi pia kukutana na Balozi wa Ubelgiji, Mhe, Paul Cartier.
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhe. Inj. Gerson Lwenge akizungumza na Balozi wa Misri, Mhe. Yasser Ahmed Al Eldin Elshawaf.
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhe. Inj. Gerson Lwenge akiwa kwenye mazungumzo na Balozi wa Misri, Mhe. Yasser Ahmed Al Eldin Elshawaf na Mkurugenzi wa Rasilimali za Maji, Hamza Sadiki.
  Balozi wa Misri, Mhe. Yasser Ahmed Al Eldin Elshawaf akimpa zawadi Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhe. Inj. Gerson Lwenge.
  Balozi wa Denmark, Mhe. Einar H. Jensen akisaini Kitabu cha Wageni, kwenye ofisi ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji, akiwa na msaidizi wake, Kansela wa Uchumi na Usimamizi wa Fedha za Umma , Mette Melson.
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhe. Inj. Gerson Lwenge akiwa na Balozi wa Denmark, Mhe. Einar H. Jensen.


 Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhe. Inj. Gerson Lwenge, Balozi wa Denmark, Mhe. Einar H. Jensen na Mkurugenzi wa Maji Mijini, Inj. Dkt. Justus Rwetabula.

No comments: