Wadhamini wa jezi wa Man United, Adidas watoa ya moyoni, yapo hapa - LEKULE

Breaking

5 Jan 2016

Wadhamini wa jezi wa Man United, Adidas watoa ya moyoni, yapo hapa

adiddas
Mkurugenzi Mtendaji wa Adidas, Herbert Hainer.


Wadhamini wa Manchester United ambao ndiyo wanaoitengenezea klabu hiyo jezi, Adidas wametoa maoni yao kuhusu mwenendo wa klabu hiyo na kusema kuwa hawafurahishwi na aina ya uchezaji ya klabu hiyo ambayo wanaamini haiwavutii mashabiki wa soka.
Kampuni hiyo ya kutengeneza vifaa vya michezo ya Ujerumani ambayo imeingia mkataba na Manchester United wa miaka 10 wenye thamani ya Pauni Milioni 750 wameyasema hayo kupitia Mkurugenzi Mtendaji wa Adidas, Herbert Hainer kuwa aina ya uchezaji wa Man United sio ambao wao wamekuwa wakiutaka.
Alisema licha ya kuwa katika kipindi kigumu lakini wanamatumaini klabu hiyo itarudi katika ubora wake wa awali na licha ya kuwa na kipindi kigumu lakini bado kampuni hiyo imekuwa na mauzo mazuri ya jezi za Man United jambo ambalo lilikuwa hawalitegemei.
“Biashara na Manchester United inakwenda vizuri, tunauza t-sherti zaidi ya tulivyofikiria tunaridhishwa na hilo licha ya kuwa hatupendezwi na mfumo ambao Man United wanacheza sio ambao sisi tunataka kuuona,” alisema Hainer.

Manchester United kwa sasa imekuwa katika kipindi ambacho kimekuwa hakiwaridhishi mashabiki wengi wa klabu hiyo kutokana na aina ya matokeo ambayo imekuwa ikiyapata ambapo katika michezo 15 imeyopita imefanikiwa kupata magoli 12 pekee hali inayopelekea mashabiki kadhaa kutaka kocha wa klabu hiyo, Louis Van Gaal kutimuliwa kazi.

No comments: