Simba wa kushangaza aliyeuawa Marekani - LEKULE

Breaking

17 Jan 2016

Simba wa kushangaza aliyeuawa Marekani

SimbaSimba huyo alikuwa pia na masharubu ya ziada
Simba wa milimani aliyeuawa katika jimbo la Idaho, nchini Marekani ameshangaza wengi kutokana na hali kwamba alikuwa na meno ya ziada kichwani.
Meno hayo kamili yanachomoza kutoka kwenye paji la uso na kuonekana kama pembe.
Simba huyo aliuawa na wawindaji walioidhinishwa tarehe 30 Desemba.
Idara ya Wanyamapori na Samaki ya Idaho imesema meno hayo huenda ni masalio ya pacha ambaye labda alifariki akiwa tumboni, au labda inatokana na saratani.
Wataalamu wa vimbe katika jimbo hilo wanasema hawajawahi kuona ulemavu wa aina hiyo awali.
Simba huyo aliwindwa na kuuawa baada ya kumshambulia mbwa karibu na mji wa Weston. Mbwa huyo alinusurika lakini mwindaji akatumwa kumuwinda simba huyo na kumuua.
Afisa wa uhifadhi wa wanyama alikagua mzoga wa simba huyo kama ilivyo sheria na ndipo akagundua meno hayo.
Mnyama huyo pia alikuwa na masharubu kwenye paji la uso kushoto.

No comments: