Matokeo ya mechi aliyohaidi Madee kuchoma gari yake moto kama Arsenal itafungwa (+Pichaz&Video) - LEKULE

Breaking

24 Jan 2016

Matokeo ya mechi aliyohaidi Madee kuchoma gari yake moto kama Arsenal itafungwa (+Pichaz&Video)

Jumapili ya January 24 Ligi Kuu Uingereza iliendelea kwa michezo miwili kupigwa, mchezo wa kwanza kuchezwa ulikuwa mchezo kati ya Everton dhidi ya Swansea City mchezo ambao ulimalizika kwa Swansea kuibuka na ushindi wa goli 2-1 licha ya kuwa katika uwanja wa ugenini.
4928
Mchezo wa pili ulikuwa ndio mchezo ulioteka hisia za watu wengi zaidi wa jiji la London, kwani ulikuwa unazikutanisha timu za jiji moja Arsenal dhidi ya Chelsea katika uwanja wa Emirates, hisia za mchezo huo hazikuishia Ulaya pekee, Tanzania msanii wa Bongo Fleva Madee Ali alitangaza kuwa kama endapo Chelsea itaifunga Arsenal basi atachoma moja kati ya magari yake moto,
5184
Kwa bahati mbaya licha ya kuwaArsenal walikuwa na mwenendo mzuri katika Ligi msimu zaidi ya Chelsea, walikubali kipigo cha goli 1-0 kutoka Chelsea wakiwa katika uwanja wao wa nyumbani. Goli la Chelsea lilifungwa na Diego Costa dakika ya 23, goli hilo lilipelekea Madee kutopatikana hewani. Kwa matokeo hayo Chelsea wanatimiza point 28 na kuwa nafasi ya 13, wakati Arsenal wameshuka hadi nafasi ya tatu wakiwa na point 44.
3561
Video ya goli la Diego Costa


No comments: