D’banj awajibu wanaoziona nyimbo zake za kipumbavu - LEKULE

Breaking

10 Jan 2016

D’banj awajibu wanaoziona nyimbo zake za kipumbavu



Rukielnino6-1
Staa wa muziki kutoka Nigeria, D’Banj.

STAA wa muziki kutoka Nigeria, D’BanjSTAA wa muziki kutoka Nigeria, D’Banj amewajibu mashabiki wake wengi wanaomponda nyimbo zake kuwa amekuwa akiimba kipumbavu tangu alipojiondoa kwenye Lebo ya Don Jazzy (Mavin Records).

Mmoja wa mashabiki wake alisema kuwa;
“D’Banj ni bonge la tajiri lakini asilimia 70 ya nyimbo zake tangu ameondoka kwa Don Jazzy zimekuwa za kipumbavu. Simaanishi kama D’Banj ni mbaya hapana! Ila nyimbo alizokuwa akiziimba kipindi yupo kwa Don Jazzy zilikuwa nzuri.”

D’Banj hakutaka kuonesha mwenye hasira baada ya kusikia maneno hayo, alichoamua ni kutengeneza njia ya mawasiliano na kuwauliza mashabiki kwa nini mtu huyo anamsema pembeni wakati hata hajaamua kuwa rafiki wake kwenye mitandao ya kijamii.

“Najua maneno yote haya, hajaniomba hata urafiki wa kwenye mitandao unajua kwa nini#Emergency.”

Emergency ni Wimbo mpya wa D’banj alioutua hivi karibuni.

No comments: