Tano Bora ya Hoteli za Kitalii Tanzania - LEKULE

Breaking

14 Dec 2015

Tano Bora ya Hoteli za Kitalii Tanzania

Ukiachana na hifadhi za taifa zitakazokufanya usichoke kutembelea miji na mikoa mbali mbali ndani ya Tanzania, ni uwepo wa hoteli za kifahari zenye utofauti wa kipekee na hoteli za nchi nyingine.
Jovago Tanzania, wadau wanaohusika na masuala ya Hoteli kimataifa, wanapenda  kuorodhshea tano bora ya hoteli zilizo kwenye chati ya kukupa mandhari zuri ya kiutalii wa kifahari hapa Tanzania.





1.Manta Resort-Pemba
Untitled 1
Ni hoteli ya kipekee yenye chumba cha kulala chini ya bahari ya Hindi. Hoteli hii inakupa mandhari ya peponi utakapo jaribu kukaa ndani ya chumba hicho, hii ni moja ya utalii ambao hutaweza kuusahau utembeleapo eneo hili kisiwani Pemba.




2.Essque Zalu Zanzibar.
Untitled 2
Essque Zalu ipo Zanzibar, ni hoteli bora ya kimataifa yenye viwango vya huduma kwa hali ya juu (five star). Ni sehemu pekee itakayokupa historia nzima ya Zanzibar na fursa ya kutembelea fukwe kubwa nzuri zinazopatikana  maeneo ya Nungwi. Imejengwa kwa nakshi za kishwahili na za kisasa za kuvutia.





3.Singita sasakwa Lodge –Serengeti
Untitled 3
Eneo lake ni zaidi ya ekari 300,000. Hoteli inavyumba vilivyojengwa kwa mandhari ya kitamaduni za kiafrika,  na uwezo wa  kuona madhari ya hifadhi ya taifa na mbuga ya wanyama Serengeti.






4.Park Hyatt –Zanzibar
Untitled 4
Ni hoteli inayokupa mandhari kamili na historia ya Zanzibar, hoteli imezungukwa na bahari ya Hindi  katika eneo la kihistoria la Stone town.




5.Hyatt Regency- Dar es Salaam.
Untitled 5

Hii ni hoteli yenye kiwango cha juu cha ubora wa kimataifa (Five star), inauwezo wa kubeba watu wengi zaidi ya hoteli yoyote Dar es Salaam. Inamandhari nzuri ya bahari ya Hindi, na vyumba vilivyojengwa kwa teknolojia ya hali ya juu, inafaa zaidi kwa masuala ya makazi  kwa mikutano ya  kibiashara pia inakupa fursa ya kutembelea  sehemu tofauti tofauti zilizo  katikati ya mji wa Dar es salaam.

No comments: