Taarifa Kwa Umma Juu Ya Wito Wa Kutoa Maoni Kuhusu Sheria Ya Ununuzi Waumma, Sura Ya 410 - LEKULE

Breaking

15 Dec 2015

Taarifa Kwa Umma Juu Ya Wito Wa Kutoa Maoni Kuhusu Sheria Ya Ununuzi Waumma, Sura Ya 410

 
WITO WA KUTOA MAONI KUHUSU SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA, SURA YA 410
_________________________
1.0     Utangulizi
Kama inavyofahamika, Sheria ya Ununuzi wa Umma inayotumika sasa, Sura ya 410, ilitungwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano mwaka 2011 kwa lengo la kuweka mfumo wa kisheria na kitaasisi wa usimamizi wa ununuzi wa umma.
 
Katika utekelezaji wa Sheria hiyo, Serikali na taasisi zake zimebaini kasaro  ambazo zimekuwa kikwazo katika utekelezaji bora wa Sheria hiyo tangu ilipotungwa kwa mara ya kwanza mwaka 2001.
 
 Kasoro zimeendelea kuwepo hata baada ya Bunge kuifuta na kutungwa upya Sheria ya Ununuzi wa Umma mwaka 2004.  Kasoro hizo ni pamoja na mlolongo mrefu na gharama nyingi katika mchakato wa ununuzi kabla ya kufanya ununuzi unaokusudiwa.
2.0     Madhumuni ya Utafiti
Kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 8(1) na (2) cha Sheria ya Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania, Sura ya 171, na Hadidu za Rejea zilizotolewa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Tume inafanya utafiti kwa lengo la:
 
(i) Kubainisha upungufu katika utekelezaji wa Sheria
(ii)kubainisha  madhara ya upungufu huo katika utekelezaji wa Sheria kwa Serikali na taasisi zake

Baada ya kukamilisha Utafiti, Tume itawasilisha Taarifa yenye Mapendekezo ya namna ya kuiboresha Sheria ya Ununuzi wa Umma ili kuleta tija katika sekta ya Ununuzi wa Umma.
 
3.0 Maoni na Mapendekezo ya Wananchi
Ili kuwezesha kufanyika kwa utafiti huo kikamilifu na kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 10 (1) (2) cha Sheria ya Tume ya Kurekebisha Sheria, Sura ya 171, Tume inatoa wito kwa watu binafsi, taasisi za Serikali na taasisi binafsi kushiriki katika kutoa maoni na mapendekezo kuhusu masharti yaliyomo katika sheria ya Ununuzi wa Umma mya mwaka 2011 na Kanuni za Ununuzi wa Umma zilizoandaliwa chini ya Sheria hiyo kwa lengo la kuiboresha.  
 
Maoni na Mapendekezo yanaweza kuwa ya jumla au kuhusu masharti mahsusi ya Sheria au mifumo ya kitaasisi iliyoundwa na Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura ya 410, kwa kuzingatia mambo yafuatayo:
  1. (i)   Misingi ya soko, pamoja na mabadiliko endelevu ya kisheria (Market fundamentals and dynamics of law)
  2. (ii)  Hatua mbalimbali katika mchakato wa ununuzi wa bidhaa au huduma (procurement process and procedural and institutional requirements)
  3. (iii)  Ulinganifu wa thamani ya fedha kwa bidhaa inayonunuliwa au huduma inayotolewa (Value for money)
  4. (iv) Mgongano unaojitokeza katika sheria  zinazohusiana na ununuzi wa umma (Conflict of laws) 
  5. (v)   Athari za kibinadamu  katika mchakato wa ununuzi kama vile rushwa, mgongano wa maslahi binafsi na ukosefu wa maadili (Human factors)
 
4.0     Muda wa Kupata Maoni/Mapendekezo
Ili kukamilisha Utafiti huu mapema, Tume imeweka muda wa siku thelathini, kuanzia tarehe 15 Desemba, 2015 hadi tarehe 14 Januari 2016 za kupata maoni na mapendekezo kutoka kwa Wananchi na taasisi husika.
 
5.0     Namna ya Kutuma Maoni/Mapendekezo
Maoni na Mapendekezo yanaweza kuwasilishwa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania kupitia njia zifuatazo:
 
Anuani ya barua
Katibu Mtendaji,


Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania,
S.L.P. 3580,
DAR ES SALAAM


Simu ya Mezani
Simu: +255 22 2123533/2111387


Nukushi
Fax: 255 22 2123534


Barua pepe


          Mtandao wa Kijamii


Tovuti


    Imetolewa na:                                  


Casmir S. Kyuki

KATIBU MTENDAJI

No comments: