Masanja Mkandamizaji Kuwania Ubunge Jimbo La Ludewa. - LEKULE

Breaking

6 Nov 2015

Masanja Mkandamizaji Kuwania Ubunge Jimbo La Ludewa.



Wagombea tisa akiwemo mdogo wake marehemu Deo Filikunjombe na mchekeshaji Masanja Mkandamizaji wamejitosa kuwania ubunge wa jimbo la Ludewa,Mkoani Njombe kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
 
Uchaguzi wa kumpata Mbunge wa jimbo hilo ulilazimika kuhairishwa baada ya kutokea kifo cha aliyekuwa mbunge na mgombea ubunge wa jimbo hilo kupitia CCM, Deogratius Filikunjombe.
 
Miongoni wa waliojitokeza kwenye kinyang'anyiro hicho ndani ya CCM ni mdogo wa marehemu, Phillipo Filikunjombe na msanii wa vichekesho na muimbaji wa nyimbo za Injili Emmanuel Mgaya maarafu kwa jina la 'Masanja Mkandamizaji'.
 
Na wagombea wengine ni Johnson Mgimba, James Mgaya, Zephania Jwahula, Deo Ngalawa, Dk Evaristo Mtitu na Simon Ngatuka.

No comments: