2
Mbunge mteule wa Jimbo la Mtama, Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape akisaini mkataba wa kupata vifaa vya huduma za afya mbele ya Mwambata wa Siasa wa Ubalozi wa China nchini Tanzania Mis Song Rui katika ofisi za Ubalozi wa Jamhuri ya Watu wa China.

Mbunge Mteule wa Jimbo la Mtama Ndugu Nape Nnauye ameanza kazi ya kuwatumikia wakazi wa jimbo hilo baada ya kusaini mkataba maalum na Ubalozi wa China nchini wa kusaidia vifaa vya huduma ya Afya kwa jimbo la Mtama.
 Ikumbukwe katika kampeni zake Nape aliahidi kulifanya jimbo kuwa la mfano kwa kuboresha huduma mbali mbali za kijamii ikiwemo afya na elimu.
Akibainisha juu ya tukio hilo kwa ajili ya jimbo lake, Nape ameeleza: ” Wakati nimeamua kugombea ubunge nilisema nataka kuwafanyia kazi watu wa Mtama nataka niwe mbunge wa mfano na niliwaahidi nitatatua kero zao mbali mbali na leo nimeanza  kwa upande wa huduma za afya ambapo vituo na zahanati kadhaa vitapata vifaa vya matibabu alivitaja baadhi ya vituo ni Mtama, Nyangamala, Chiponda, Namupa, Chiuta,Luo, Nyengedi,Kiwalala na kwengineko.” alimalizia Nape.