Wanawake na Watoto Waanza Kuodoka Mkoani Mtwara Wakihofia Kutokea Kwa Vurugu Baada Ya Uchaguzi - LEKULE

Breaking

22 Oct 2015

Wanawake na Watoto Waanza Kuodoka Mkoani Mtwara Wakihofia Kutokea Kwa Vurugu Baada Ya Uchaguzi


Shirika  la  utangazaji  la  Ujererumani,DW  limeripoti  leo  mchana  kuwa idadi kubwa ya watu  wameanza kuondoka  mkoani Mtwara  wakihofia hali ya usalama wakati wa uchaguzi.
 
Kwa mujibu wa Dw,watu wengi  wanaoondoka  ni wanawake na watoto, hali ambayo inaelezewa inatokana na vurugu za gesi za mwaka 2013,  kuonekana kwa baadhi ya vifaa vya jeshi na wanajeshi wakiwa kwenye vifaru.

Idadi ya watu wanaondoka katika mkoa wa Mtwara nchini Tanzania wakihofia hali ya usalama wakati wa uchaguzi imeongezeka na kuzidi kuongeza hofu katika jamii huku wengi wanaondoka katika mkoa huu ni wanawake na watoto, hali ambayo inaelezewa inatokana na kutokea kwa vurugu za gesi mwaka 2013 na kuonekana kwa baadhi ya vifaa vya jeshi na wanajeshi wakiwa kwenye vifaru.

No comments: