14 Oct 2015

Ripoti:Thomas Sankara aliuwawa kinyama



Thomas Sankara
Matokeo ya ukaguzi wa kimatibabu uliofanyiwa mabaki ya mwili wa aliyekuwa rais wa Burkina Faso marehemu Thomas Sankara miaka 28 baada ya kuuawa,yanaonyesha kuwa mwili wake ulijaa risasi kulingana na wakili aliyekuwa akiwakilisha familia yake kulingana na mtandao wa facebook wa kituo cha habari cha Burkina 24.
Familia yake ilikuwa ikingojea matokeo ya DNA kuthibitisha kwamba mabaki hayo yalikuwa ya bwana Sankara,wakili Benewende Sankara aliviambia vyombo vya habari nchini humo.

Mariam Sankara mkewe marehemu Thomas Sankara
Bwana Sankara aliuawa katika mazingira ya kutatanisha akiwa na umri wa miaka 37 na kundi la wanajeshi mwezi Octoba mwaka 1987,na alizikwa kwaa haraka kufuatia mpainduzi yalioongozwa na mrithi wake Blaise Compaore.BBC

No comments:

Post a Comment