Uwoya Awashangaa Wasanii Wasioisapoti CCM - LEKULE

Breaking

18 Sept 2015

Uwoya Awashangaa Wasanii Wasioisapoti CCM


Mrembo wa filamu za kibongo nchini ambaye ameshapitishwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwania ubunge wa viti maalumu, Irene Uwoya anawashangaa wasanii wenzake ambao hawakiungi mkono chama hicho wakati baadhi yao walikuwa karibu sana na Rais Jakaya Kikwete anayemaliza muda wake.
 
Kupitia mtandao wake wa kijamii wa Instagram, Uwoya amewachana wasanii ambao wamekuwa wakisema hawaoni sababu ya kumuunga mkono wakati yeye hakuwahi kuwathamini hata siku moja.
 
“Sasa narudi kwa wasaniii wasio jitambua! katika tasnia yetu, ukweli usiopingika Kikwete amekuwa karibu sana na wasanii na ametufanya tuthaminike.
 
“Lakini chaajabu kunawatu wanajifanya hawajui mchango wake, kiukweli inaumiza sana!
 

"Kuna watu walikuwa wanashinda Ikulu , anawasaidia sana katika kazi zao lakini leo wamesahau yote na kumsapoti mtu ambaye hajawahi hata kuwatambua kwanafasi zao, kama sio ushabiki maandaz niniii? Loooo!!! aibu”.Uwoya ameandika.

No comments: