Sheikh Mkuu amethibitisha Watanzania kufariki Saudi Arabia…RIP - LEKULE

Breaking

25 Sept 2015

Sheikh Mkuu amethibitisha Watanzania kufariki Saudi Arabia…RIP


September 24 2015 imeripotiwa Taarifa kuhusu watu zaidi ya 700 kufariki kwenye Msikiti Mkuu wa Hijja ambao uko Mecca, Saudi Arabia.
Taarifa imetolewa na Mufti Mkuu wa Tanzania aliyeko huko Sheikh Abubakar Zuber ambae nae yuko Mecca ambao walienda kwa ajili ya Hijja, kwenye Taarifa hiyo yametolea majina pamoja na idadi ya Watanzania ambao wamefariki na kujeruhiwa.
Watanzania waliotajwa kufariki ni watu watano pamoja na Raia mmoja wa Kenya.
Watanzania waliofariki na kutambulika majina yao ni Bi Mwanaisha JumaMkungwe Suleiman na Seif Said… jina la Raia mmoja wa Tanzania halitambulika, na Raia wa Kenya aliyefariki ni Bi. Fatuma Mohammed.
Amesema katika kipindi hiki wanaendelea kufanya mawasiliano na Wizara husika wakishirikiana na ubalozi wa Tanzania kupata taarifa zaidi kama kuna wengine walioathirika katika tukio hilo huku Serikali ya Saudi Arabia ikiendelea na zoezi la kutambua uraia wa kila mwili na kutoa taarifa kwa nchi husika.