NITABORESHA MASLAHI YA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA-MAGUFULI - LEKULE

Breaking

10 Sept 2015

NITABORESHA MASLAHI YA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA-MAGUFULI



Msafara wa Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli ukiwasilia katika mkutano wa hadhara wa kampeni,Korogwe vijijini.
MGOMBEA urais kwa teketi ya CCM, Dk.John Magufuli akifafanua jambo kwa msisitizo huku akibainisha kuwa iwapo atachaguliwa kwenye uchaguzi mkuu mwaka huu, basi Serikali yake itahakikisha inaboresha maslahi ya watumishi wa majeshi ya ulinzi na usalama nchini kutokana na kutambua mchango wao katika kulinda amani ya nchi yetu.
Dkt Magufuli alisema kuwa anataka kuona watumishi wa jeshi hilo wanakuwa na mishahara
mizuri na hiyo itawezesha kufanya kazi ya ulinzi na usalama wa nchi kwa ufanisi zaidi huku akitumia nafasi hiyo kuomba Watanzania kudumishaamani ya nchi kwani ikipotea hakutakuwa na maendeleo ya aina yoyote.
Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli pamoja na Mgombea Ubunge wa jimbo la Bumbuli wakiwaaga wananchi wa Bumbuli waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika mjini humo jioni ya leo.
Wakazi wa Jimbo la Bumbuli wakifuatilia kwa makini mkutano wa Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli alipokuwa akiwahutubia jioni ya leo.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa kata ya Magoma wakati akiwa njiani kuelekea Korogwe mjini kwenye mkutano wa kampeni za CCM.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wa Mashewa wilayani Korogwe kwenye mkutano wa kampeni za CCM ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa serikali yake itakuwa ya kuchapa kazi kwa maendeleo ya wananchi na nchi kwa jumla.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akimkabidhi Ilani ya CCM pamoja na kumnadi mgombea Ubunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini Ndugu Stephen Ngonyani kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Kwamazandu, Korogwe Vijijini.
Bangozzzz
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akimkabidhi mgombea ubunge wa Jimbo la Korogwe mjini  Mary Chatanda Ilani ya uchaguzi ya CCM kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika viwanja vya chuo cha ualimu Korogwe.
Mwenyekiti wa Wazazi CCM Taifa,Ndugu Bulembo akimkaribisha mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli kuwahutubia wananchi katika uwanja wa Togotwe-Mponde wilayani humo.
Wakazi wa Bumbuli waliojitokeza kwa wingi wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye mkutano wa kampeni wa CCM jioni ya leo,
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa Bumbuli kwenye viwanja vya Togotwe ambapo aliwaahidi kuwajengea barabara ya lami pamoja na kufuatilia suala la kiwanda cha Chai cha Mponde.
 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa Bumbuli kwenye viwanja vya Togotwe ambapo aliwaahidi kuwajengea barabara ya lami pamoja na kufuatilia suala la kiwanda cha Chai cha Mponde.
Wananchi wakifuatilia mkutano.
Mgombea Ubunge jimbo la Bumbuli Mhe. January Makamba akifafanua jambo mbele ya umati wa wananchi  wa Jimbo hilo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Togotwe.
Wananchi wa Lushoto mjini wakishangilia jambo mara baada ya kumsikia Mgombea Urais wa CCM,Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia 

No comments: