11947662_1042542635758794_8488837271287773925_nMgombea Ubunge jimbo la Kigamboni  kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akipeperusha benndera ya UKAWA, Kamanda Lucy Magereli 

(Kigamboni-Dar es Salaam) Mgombea Ubunge kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia anapeperusha bendera ya UKAWA inayoungwa mkono na vyama vya NCCR-Mageuzi, NLD, CHADEMA na CUF, Kamanda Lucy Magereli  amewataka wananchi wa jimbo hilo la Kigamboni kumpigia kura za ndio  hiyo Oktoba 25, mwaka huu ili aweze kwenda kutetea kero zao mbalimbali.
Lucy Magereli anaeleza kuwa, wananchi wa jimbo hilo wanataka mabadiliko hasa kwa kupelekewa maendeleo na si porojo kama wafanyavyo Chama tawala ambacho kimeshindwa kuwatetea kwa zaidi ya miaka mingi huku kikiendelea kuwanyonya na hata kupokonya haki zao ikiwemo Ardhi. Pia imeshindwa kutekeleza huduma bora za kielimu, Afya na miundombinu zaidi ya miaka mingi huku hata wakipeleka huduam hizo ni chini ya kiwango.
“Kila mwana Kigamboni. wakati wa mabadiliko ni huu. Oktoba 25, mapema naomba kura yako..Tuichague CHADEMA kwani ndio mkombozi wa kweli na Mabadiliko tunayoyataka ni sasa” alieleza Lucy Magereli.
Lucy Magereli anaendelea kuchanja mbuga katika maeneo mbalimbali ya Jimbo hilo la Kigamboni huku akiwatak wananchi kujitokeza kwa wingi kusikiliza sera na kumuunga mkono.
11990378_1041620125851045_7738030136105089065_nMgombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Kigamboni kwa tiketi ya CHADEMA na UKAWA, Kamanda Lucy Magereli (wa pili kutoka kushoto) akiwa katika mkutano wa Kampeni katika Kata ya Kisarawe hivi karibuni…
11954623_1040623119284079_7014782049246866828_nCHADEMA mwendo mdundo Kigamboni…. baadhi ya wafuasi wa Chadema wakiwa katika mkutano wa Kigamboni kumsapoti Kamana Lucy Magereli.. hivi karibuni.
11951777_1041620055851052_1719736022330967114_n
Chadema mwendo mdundo Jimbo la Kigamboni…