utalii 1
Ni siku chache tu zimepita, Tanzania imesheherekea siku ya utalii duniani kwa kauli mbiu Mamilioni ya watalii ni mamilioni ya fursa” ambapo kauli mbiu hii imekuwa na lengo zuri la kuweka vipaumbele vya kimaendeleo katika sekta ya utalii Tanzania.
Tanzania, kati ya nchi za Umoja wa Mataifa, huadhimisha siku kuu hii kila tarehe 27 ya mwezi Septemba ya kila mwaka, kwa lengo kubwa la kuhamasisha uelewa juu ya sekta ya utalii na mchango wake katika jamii.
Ban Ki-moon, Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa alifafanua kwamba, “utalii unaleta fursa nyingi kwa kuajiri watu wengi na kukuza uchumi wa nchi kupitia mabilioni ya watalii wa kimataifa wanaosafiri kila mwaka”. (Redio ya Umoja wa Mataifa)
Hata hivyo, Tanzania imekuwa ikishehereka siku kuu hii kila mwaka, lakini bado kumekuwa na ufahamu mdogo kuhusiana na sekta hii ya utalii hasa kwa watanzania wasio na desturi ya kutembelea maeneo ya hifadhi ya taifa. 
utalii 2
“Kwa kuwa asilimia 33 ya eneo la nchi ni maeneo yaliyohifadhiwa kisheria ikiwemo misitu na wanyamapori, Tanzania inabidi iwe mstari wa mbele katika ufuatiliaji wa kauli mbiu hiyo ikiwemo  kuboresha sehemu muhimu kama hoteli za kitalii na hifadhi za taifa kwa kuangalia kama zinakidhi viwango vya kushindanishwa na  nchi za jirani”. Andrea Guzzoni,Meneja mkazi wa JovagoTanzania aliafafanua.
Hata hivyo bado tunahitaji kuangangalia changamoto nyingine nyingi zinazoikabili sekta hii, ikiwemo ujangili na biashara haramu ya nyara, migogoro ya mipaka na uvamizi wa maeneo ya hifadhi ya taifa, pamoja na uhaba wa elimu ya kutosha juu ya utunzaji wa misitu na hifadhi za taifa, alifafanua.
utalii 3
Kwa upande wake Lilian Kisasa, Afisa meneja mawasiliano wa JovagoTanzania aliongeza kwa kusema kuwa, “mwisho wa kauli mbiu hii sio siku ya utalii duniani peke yake, inabidi kutilia mkazo hasa katika utendaji wa kazi kuanzia ngazi ya familia, kijana au jami kwa ujumla itambue kuwa sekta hii ni utambulisho tosha wa madhari na sura ya taifa yetu. Serikali na sekta binafsi ni jukumu letu kuhakikiksha miundo mbinu kama barabara, viwanja vya ndege, na madaraja kwa mwaka 2016 ziwe katika sura mpya”.