KITUO CHA UFUATILIAJI WA UCHAGUZI TANZANIA (CEMOT) CHAZINDULIWA - LEKULE

Breaking

3 Sept 2015

KITUO CHA UFUATILIAJI WA UCHAGUZI TANZANIA (CEMOT) CHAZINDULIWA



Kutoka kushoto ni viongozi wa CEMOT, Meneja mradi, Bernard Kindoli na Balozi wa Den mack, Etnar Jensen.

Kutoka kushoto ni Mwenyekiti mwenza kutoka Tanzania Civil Society Consortium on Election Observation (TACCEO), Martina Kabisama, Meneja mradi, Bernard Kindoli na Balozi wa Den mack, Etnar Jensen.

Wanahabari wakifuatilia mkutano huo.

Balozi wa Den mack, Etnar Jensen akitoa ufafanuzi baada ya kuulizwa maswali na wanahabari. (P.T)
Asasi za kiraia zinazofuatilia na kuangalia chaguzi nchini Tanzania zimeunda muungano unaoitwa Coalition on Election Monitoring and Observation in Tanzania kwa kifupi CEMOT. CEMOT inaendeshwa kwa ushirikiano baina ya TEMCO (Tanzania Election Monitoring Committee) na TACCEO (Tanzania Civil Society Consortium for Election Observation). Lengo kuu la CEMOT ni kuongeza ushiriki wa wananchi katika kufuatilia na kuangalia mchakato wa uchaguzi ili kuwa na fursa ya kuhakikisha uhalali (credibility) wake.
Kwa kuwa CEMOT inakusudia kutumia teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) katika kupata taarifa mbali mbali za matukio yanayohusu uchaguzi kutoka kwa waangalizi wa ndani na wananchi kwa ujumla, imetengeneza Kituo cha Ufuatiliaji wa Uchaguzi (Tanzania Election Observation Centre).
Lengo kuu la kituo hiki ni kuongeza ushiriki wa wananchi katika kufuatilia na kuangalia Uchaguzi Mkuu wa 2015. Pia ni kuwapa wananchi fursa ya kuwasiliana moja kwa moja na taasisi za Serikali zinazohusika na usimamizi wa uchaguzi. Taasisi hizo ni kama vile Tume ya Uchaguzi ya Taifa, Tume ya Uchaguzi Zanzibar, Jeshi la Polisi, Kamisheni ya Polisi Zanzibar, Ofisi ya Msajili wa Vyama, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi Zanzibar, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Seriali, na nyinginezo.
CEMOT inaamini kuwa kwa kufikisha taarifa kwa wakati kwa wadau na mamlaka za uchaguzi kutadumisha utulivu na maelewano kabla, wakati na baada ya uchaguzi.Ufunguzi wa kituo cha CEMOT cha Ufuatiliaji wa Uchaguzi unaofanyika kuanzia leo Septemba 2, 2015 kuanzia saa tisa mchana katika ukumbi wa Hoteli ya Southern Sun Dar es Salaam.
Uzinduzi huo utahudhuriwa na wadau wa uchaguzi wa ndani na nje ya nchi, wachambuzi nguli wa masuala ya uchaguzi, waangalizi wa ndani na nje pamoja na wanachi waalikwa. Pia kutakuwa na mabalozi wa nchi mbalimbali pamoja na wawakilishi wa taasisi zinazoshugulika na uangalizi wa uchaguzi.
CEMOT inaamini kituo hiki kitasaidia kusaidia kuboresha mchakato wa uchaguzi wa mwaka 2015 na chaguzi nyingine zitakazofuata kwa kutoa fursa kwa wananchi kuwasiliana moja kwa moja na vyombo husika kunapokuwa na tatizo.
Kituo hiki kinatarajia kufanya kazi kwa kushirikiana na waangalizi wa uchaguzi wa muda mfupi wapatao 10,000 katika vituo mbalimbali, waangalizi wa uchaguzi wa muda mrefu wapatao 350, timu za wataalamu wa TEHAMA pamoja na wachambuzi wa uchaguzi kwenye uwanda wa siasa, sharia, habari, na jinsia.
Kituo hiki cha kidigitali kitapatikana katika wavuti ya www.uchaguziwetu2015.org pamoja na
Twitter: uchaguziwetu15
Facebook: uchaguziwetu2015
Instagram: uchaguziwetu2015
Youtube: uchaguziwetu2015
Kauli mbiu yetu ni: andaa, shirikisha na jishirikishe kwa uchaguzi wenye uhalali, huru na haki (generate, share, engage. credible, free and fair elections)
Shughuli ya Uzinduzi wa Kituo cha Ufuatiliaji wa Uchaguzi, utatanguliwa na ufunguzi wa ofisi za CEMOT zilizopo katika Jengo la GEPF barabara ya Ali Hassan Mwinyi (mkabala na kituo cha mafuta cha Victoria), Ghorofa ya Saba.
Imetolewa na
CEMOT
Kitengo cha Habari na Mawasiliano
02.09.2015

No comments: