KIKWETE AMEZITAKA NCHI ZA AFRIKA KUIPA NGUVU MAHAKAMA YA AFRIKA ILI IWEZE KUSIKILIZA KESI ZA JINAI - LEKULE

Breaking

14 Sept 2015

KIKWETE AMEZITAKA NCHI ZA AFRIKA KUIPA NGUVU MAHAKAMA YA AFRIKA ILI IWEZE KUSIKILIZA KESI ZA JINAI

87df3-jk


Raisi Jakaya Kikwete amewataka viongozi wa nchi za Afrika kuipa nguvu mahakama ya Afrika ya Haki za binadamu iliyoko jijini Arusha ili iweze kusikiliza za kesi za  jinai badala ya kupelekwa moja kwa moja kwenye mahakama ya kimatifa ya makosa ya jinai.
Kikwete amesema kuwa  iwapo Mahakama hiyo itapewa nguvu itarahisisha upatikanaji wa haki za raia katika bara la Afrika na kuimarisha misingi ya utawala bora na kuheshimu haki za Binadamu.
Akihutubia Mahakama hiyo jana Raisi Kikwete  alizindua kitabu chenye  taarifa muhimu za mahakama hiyo kilichoandikwa kwa lugha ya Kiswahili ,amesema kuwa ni hatua mojawapo katika kuhakikisha lugha hiyo inatumika mahakamani hapo na kuwawezesha Watanzania wengi na Waafrika kuelewa shughuli za mahakama hiyo na utendaji kazi wake.

Raisi wa Mahakama hiyo Jaji Agustino Ramadhani amesema kuwa itachukua muda mrefu kwa mahakama hiyo kuanza  kusikiliza  kesi za jinai kwani bado nchi nyingi za Kiafrika hazijaidhinisha mkataba wa Malabo uliotolewa tangu Juni mwaka jana  ili kuanzisha hatua za usikilizwaji wa kesi za jinai.
“Mpaka sasa hakuna nchi hata moja iliyoidhinisha mkataba wa Malabo ambao ulitolewa tangu juni mwaka jana hivyo itachukua muda mrefu mpaka mahakama iweze kusikiliza kesi za jinai” Alisema Jaji Ramadhani


Ziara ya Raisi Kikwete kutembelea Mahakama hiyo imetajwa kuwa ziara ya Mwisho ya Raisi huyo katika kipindi cha Uongozi wake unaolekea tamati  lakini pia ni ziara ya kwanza ya Rais huyo tangu kuanzishwa kwa Mahakama ya Afrika.

No comments: