FAINALI YA MCHEZO WA BAO NA KARATA EACROTANALI ZANZIBAR - LEKULE

Breaking

27 Sept 2015

FAINALI YA MCHEZO WA BAO NA KARATA EACROTANALI ZANZIBAR


 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akicheza bao la kete na mzee Abdalla Salim Kitambo wa Wilaya ya Mjini wakati alipofika kuyafunga mashindano ya fainali ya mchezo huo na mchezo wa Karata katika viwaja vya Eacrotanal leo

 Baadhi ya Timu mbali mbali za Michezo ya Bao la Kete na karata wakiwa katika fainali ya michezo hiyo iliyofanyika leo katika viwanja vya Eacrotanal Mjini Unguja,wakati mgeni rasmi akiwa  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
 Timu za mchezo wa karata kutoka kibanda mawazo Miembeni Chake chake Pemba na kwamtipura Unguja zikichuana katika fainali iliyofanyika leo katika viwanja vya Eacrotanal Mjini Unguja,mbele ya mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akizungumza na vikundi mbali mbali vya michezo ya bao na karata wakati wa fainali ya michezo hiyo iliyochezwa leo katika viwanja vya Eacrotanal Mjini Unguja
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein  akimkabidhi kombe bingwa wa mchezo wa Bao la Kete Kidodi Salum Kidodi wa klabu ya Mwembeladu baada ya kumfunga mpinzani wake katika fainali Mzee Nassor Othman wa klabu ya Bora imani ya Jangombe wilaya ya Mjini  iliyochezwa leo katika viwanja vya Eacrotanal Mjini Unguja
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein  akimkabidhi kombe bingwa wa mchezo wa Bao la Kete Kidodi Salum Kidodi wa klabu ya Mwembeladu baada ya kumfunga mpinzani wake katika fainali Mzee Nassor Othman wa klabu ya Bora imani ya Jangombe wilaya ya Mjini  iliyochezwa leo katika viwanja vya Eacrotanal Mjini Unguja
 [Picha na Ikulu.]