Bendera ya Palestina kupepea ofisi za UN - LEKULE

Breaking

11 Sept 2015

Bendera ya Palestina kupepea ofisi za UN

Bendera ya Palestina

Baraza kuu la Umoja wa mataifa limepiga kura muswada kuipa fursa ya kipekee na kutoa baraka zake kuiruhusu bendera ya Palestina kupepea mbele ya majengo ya Umoja wa Mataifa .
Chini ya azimio hilo ambalo yalilopitishwa, bendera za mataifa mawili ambayo si mataifa kamili ambayo ni watazamaji wa umoja huo Palestina na Holy See ,sasa watakuwa na ruhusa ya kupeperusha bendera sambamba na nchi wanachama.
Muwakilishi wa Palestina katika Umoja wa Mataifa, Riyad Mansour,amesema kwamba tukio hilo ni hatua kubwa kuimarisha heshima ya nchi yake .

Lakini Israel imesema hatua hayo imeshusha hadhi ya umoja huo na kusisitiza kwamba njia pekee kwa Palestina kupata hazi ya kuwa taifa huru ni kupitia meza ya mazungumzo ya ana kwa ana.

No comments: