Baraza la Habari Tanzania (MCT) na Shirika la Utangazaji la BBC, Latao Mafunzo kwa Waandishi wa Habari Kisiwani Pemba. - LEKULE

Breaking

17 Sept 2015

Baraza la Habari Tanzania (MCT) na Shirika la Utangazaji la BBC, Latao Mafunzo kwa Waandishi wa Habari Kisiwani Pemba.

Waandishi wa Habari Kisiwani Pemba wapata mafunzo ya kuripoti habari za Uchaguzi kupitia Mahojiano na Viongozi wa Vyama vya Siasa na Wananchi, wakati wa kuripoti habari za Uchaguzi Mkuu Zanzibar unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi October 2015, Wakimsikiliza Mkufunzi wa Mafunzo hayo hayuko pichani, Bi Lilian Timbuka, kutoka MCT/BBC,akiwasilisha Mada mbili za Jinsi ya Kujiandaa katika Kufanya Mahojiano na Viongozi wa Vyama vya Siasa na Usalama wa Kuripoti Habari za Uchaguzi Zanzibar. Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa hoteli ya ZSSF Chakechake Pemba.Mafunzo hayo yameandaliwa na MCT kwa kushirikiana na BBC kwa ajili ya kuwajengea uwezo kuripoti habari za Uchaguzi Zanzibar.
Baadhi ya Waandishi wakiwa katika mafunzo hayo ya kuripoti habari za mahojiano na Usalama wao katika Kipindi cha Uchaguzi yalioandaliwa na MCT na BBC Kisiwani Pemba.
Waandishi wakiwa makini wakifuatilia Mada iliokuwa ikiwakilishwa na Muhusika wakati wa mafunzo yao ya Siku Tatu ya kuripoti habari za Uchaguzi Zanzibar, yalioandaliwa na Baraza la Habari Tanzania na Shirika la Utangazaji la BBC, kuwajengea uwezo waandishi katika kazi yao ya kuripoti habari hizo.  





Mshiriki wa mafunzo hayo Ndg Ali Bakari akichangia mada wakati wa mafunzo hayo. kwa waandishi yaliofanyika kisiwani Pemba katika ukumbi wa hoteli ya ZSSF Chakechake Pemba.
                               Baadhi ya waandishi wakifuatilia mafunzo hayo. 

Mwandishi mkongwe kisiwani Pemba Ndg Hatibu Mjaja akichangia kuhusiana na waandishi kujifunza na kujituma katika kazi yao hasa wanapofanya mahojiano na viongozi wajaribu kuwa na kumbukumbu na jitihada binafsi.
Mwandishi wa habari wa Shirika la  Utangazaji la Zanzibar ZBC Bi, Nasra Mohammed akichangia mada kuhusiana na muandishi kujiandaa wakati wa kufanya mahojiano na muhusika kuandaa maswali yake na kujiamini wakati wa kazi hiyo ili kuweza kwenda sambamba wakati wa mahojiano hayo kuepusha majibu ya ndio na hapana.

Programu Ofisa wa Baraza la Habari Tanzania kituo cha Zanzibar Bi Shifaa Hassan akifuatilia michango iliokuwa ikiwasilishwa na Waandishi wa Habari wakati wa mafunzo hayo ya kuripoti habari za Uchaguzi, Mafunzo hayo yameandaliwa na MCT na BBC kuwajengea uwezo waandishi kuripoti vizuri habari za uchaguzi bila ya kuleta sitofahamu kwa Wananchi wakati wa kipindi hicho mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa hoteli ya ZSSF Chakechake Pemba.na kuwashirikisha waandishi wa Vyombo vya Serikali na Binafsi. 

No comments: