Balozi Seif akagua kiwanja cha kufurahisha watoto cha Umoja Tibirinzi - LEKULE

Breaking

11 Sept 2015

Balozi Seif akagua kiwanja cha kufurahisha watoto cha Umoja Tibirinzi

 Muonekano wa haiba ya uwanja wa Kufurahishia Watoto wa ZSSF-Umoja Amusement Park uliopo Tibirinzi Chake Chake Pemba unavyoonekana kwa juu.

  Baadhi ya Pembea zilizomo ndani ya uwanja wa Kufurahishia Watoto wa ZSSF-Umoja Amusement Park uliopo Tibirinzi Chake Chake Pemba ambazo zitakuwa zikitoa huduma kwa wananchi wakati wa sherehe mbali mbali.
  Baadhi ya Pembea zilizomo ndani ya uwanja wa Kufurahishia Watoto wa ZSSF-Umoja Amusement Park uliopo Tibirinzi Chake Chake Pemba ambazo zitakuwa zikitoa huduma kwa wananchi wakati wa sherehe mbali mbali.
  Baadhi ya Pembea zilizomo ndani ya uwanja wa Kufurahishia Watoto wa ZSSF-Umoja Amusement Park uliopo Tibirinzi Chake Chake Pemba ambazo zitakuwa zikitoa huduma kwa wananchi wakati wa sherehe mbali mbali.
 Meneja Mipango, Uwekezaji na Utafiti wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar { ZSSF } Ndugu Khalifa  Muumin Hilal akimkaguza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif aliyefika kwenye kiwanja hicho kukagua hatua iliyofikiwa baada ya kukamilika ujenzi wake.

 Ndugu Hilal akimueleza Balozi Seif mfumo mzima wa huduma za Umeme wa Janareta inayoanza kutumika ndani ya sekunde tatu tuu endapo umeme wa kawaida unapozimika ghafla katika uwanja huo bila ya kuathiri Pembea.
 Wafanyakazi wa Uwanja wa Kufurahishia Watoto Tibirinzi wakiwa katika majaribio ya Vigari vitakavyotoa huduma kwenye uwanja huo ikiwa ni moja ya sehemu inayowavutia watoto.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi  Seif Ali Iddi akiwaagiza wafanyakazi wa uwanja wa kufurahishia watoto Tibirinzi kufanya kazi zao kwa upendo na unyenyekevu wakati wanapowahudumia watoto.



Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amewaagiza wafanyakazi wa Kiwanja cha kufurahishia Watoto cha  ZSSF - Umoja Amusement Park kiliopo Tibirinzi Chake chake Pemba kuwa waangalifu wakati wanapo hudumia Watoto   wadogo kwenye sherehe zenye  mjumuiko wa watu wengi kiwanjani hapo.

Alisema uangalifu wa watendaji hao ndio njia pekee itakayosaidia kuwatoa hofu Wazazi na Walezi pamoja na kuwapa upendo na faraja watoto wanaoamua kupata huduma za burdani na michezo mbali mbali kwenye kiwanja hicho.

Balozi Seif  alitoa agizo  hilo wakati alipofanya ziara fupi kukagua hatua ya Kiwanja hicho kilichozinduliwa hivi karibuni na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Ali Mohammed Shein ambacho kiko tayari kuanza kutoa huduma katika siku za Mapumziko, sherehe za Iddi pamoja na zile za kitaifa.



Balozi Seif alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  kupitia Taasisi zake za Umma mfano mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar { ZSSF } imeamua kujenga miundo mbinu  katika  maeneo ya wazi itakayowapa fursa Watoto wa Taifa hili kupata sehemu za burdani na mapumziko baada ya harakati zao za Kimasomo.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliupongeza Uongozi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar { ZSSF } kwa juhudi uliochukuwa wa kujenga  Viwanja vya michezo na Burdani  Unguja n a Pemba kwa lengo la kukidhi haki za Watoto hapa Nchini.

Aliwataka wafanyakazi wa Uwanja huo kuwa waangalifu katika uendeshaji wa vyombo mbali mbali  kama Pembea vilivyomo ndani ya uwanja huo ili viweze kumudu kwa kipindi kirefu ili kurejesha gharama ya fedha zilizotumika katika ujenzi wa miradi hiyo.

Alifahamisha kwamba ni vyema kwa watendaji hao kuhakikisha kwamba wanaimarisha ushirikiano wa karibu kati yao na Uongozi husika sambamba na kutoa Taarifa mapema pale inapotokezewa hitilafu miongoni mwa vyombo wanavyovihudumia  kama Pembea.

Mapema Meneja Mipango, Uwekezaji na Utafiti wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar { ZSSF } Ndugu Khalifa  Muumin Hilal alimueleza Balozi Seif kwamba  kazi iliyopo hivi sasa katika kiwanja hicho cha Tibirinzi ni kuwapatia mafunzo watendaji wa Kiwanja hicho ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa uhakika na uelewa mpana.

Nd. Muumin alisema wakati mafunzo hayo yakiendelea  huduma za michezo na Burdani kwenye kiwanja hicho zimeanza kwa siku za mapumziko za Jumamosi na Jumapili na zitaendelea kama kawaida kwenye sherehe za Siku Kiuu za Kidini pamoja na zile za Kitaifa.
Meneja Mipango, Uwekezaji na Utafiti huyo wa ZSSF alifahamisha kwamba ipo changamoto kubwa ya mazingira ya hali ya hewa inayoizunguuka sehemu hiyo inayoonyesha muelekeo wa kusababisha kufanya kutu kwa baadhi ya vyuma vya Pembea za Kiwanja hicho.

Alieleza kuwa Uongozi kupitia Wahandisi wa Kiwanja hicho watalazimika kuwa makini wakati wote katika kuvifanyia matengenezo  vifaa hivyo kwa kupata rangi ili viweze kutumika kwa muda mrefu.

Kiwanja cha kufurahishia Watoto cha  ZSSF - Umoja Amusement Park kiliopo Tibirinzi Chake chake Pemba kilichojengwa na Kampuni ya Ujenzi ya Mazrui Building Construction Limited kimegharimu Jumla ya Shilingi Bilioni Saba za Kitanzania.


Zaidi ya watu 12,000 wanaweza kuhudumiwa kwa wakati mmoja kwenye kiwanja hicho kinachotarajiwa kurejesha gharama za fedha zilizotumika katika kipindi cha miaka 12 ijayo.

No comments: