Mwanamuziki anayekimbiza kwenye game la muziki wa Kibongo, Aman Temba ‘Mh. Temba’.
MWANAMUZIKI anayekimbiza kwenye game la muziki wa Kibongo, Aman Temba ‘Mh. Temba’ siku si nyingi anategemea kuibuka na ngoma inayoitwa Fundi, aliyoifanyia katika Studio ya Mj Records chini ya produza Marco Chali na kumshirikisha mwanamitindo maarufu Bongo, Jokate.
Mwanamitindo maarufu Bongo, Jokate.
Mh. Temba aliitonya BLOG HII kuwa, wimbo huo wenye mahadhi ya
kimalavidavi ilikuwa autambulishe mapema wiki hii lakini menejimenti
yake imembania na kumtaka asubiri kwanza wamalize kushuti video.“Jokate kafanya kweli kwenye hiyo ngoma, mashabiki wasubirie kitu kizuri maana niko katika hatua za mwisho za kufanya video kwa Adam Juma, soon ikikamilika kama manejimenti ilivyotaka nitaiachie kwenye media,” alisema Temba.
No comments:
Post a Comment