Kombe la dunia:Timu 3 za Afrika zashindwa - LEKULE

Breaking

15 Aug 2015

Kombe la dunia:Timu 3 za Afrika zashindwa

Uganda ililazwa na New Zealand
Timu tatu kutoka Afrika ziliambulia kichapo katika kombe la dunia la mpira wa pete inayoendelea Sydney Australia.
Wawakilishi wa Afrika Mashariki ,Uganda, waliambulia kibano cha alama 76-33 mikononi mwa New Zealand katika hatua ya nusu fainali huko Sydney.
Kufuatia kushindwa huko Uganda sasa inajiunga na Afrika Kusini na Malawi ambazo pia hazikuwa na siku nzuri.
Afrika kusini ilikuwa imechapwa alama 62-46na Uingereza.
Afrika kusini ilikuwa imechapwa alama 62-46na Uingereza.
Malawi kwa upande wake itajilaumu yenyewe kwa kuboronga katika muda wa lala salama wa mechi hiyo baada ya kushindwa na Jamaica kwa alama moja pekee.
Malawi ilikuwa uongozini hadi dakika ya mwisho safu ya ulinzi ilipozembea na kuiruhusu Jamaica kufunga bao la kusawazisha na kisha kuwapiku.
Kufuatia kichapo hicho cha alama moja Malawi walishindwa kufuzu kwa mkumbo wa nusu fainali ya mashindano hayo.
Mataifa hayo ya Afrika yamesalia kuwania nafasi ya 5 hadi 16.
Mkufunzi wa Malawi Mary Waya ameiambia BBC michezo kuwa timu yake ndiyo iliyokuwa bora ila ilikosea tu ilipowadia wakati wa kuwa wakakamavu kisaikolojia.
Kufuatia matokeo hayo sasa Mataifa hayo ya Afrika yamesalia kuwania nafasi ya 5 hadi 16.
Mashindano hayo yanaendelea.

No comments: