KAMPUNI moja nchini China imepanga masharti kwa wafanyakazi wake wa kike ikiwa watataka kupata mimba.
Masharti hayo ambayo yamewekwa katika sheria za kampuni hiyo zimezua malalamiko mengi katika mitandao ambapo wanawake wote walio kwenye ndoa lazima wawe wamefanya kazi kwa mwaka mmoja kwenye kampuni hiyo kabla ya kutoa maombi ya kukubaliwa kushika mimba.
Kwa mujibu wa masharti hayo, anayekiuka utaratibu huo na kushika mimba bila ya idhini, atatozwa faini au hapandishwi cheo.
Shirika la utangazaji la China limekosoa vikali kampuni hiyo iliyoko mkoa wa Henan na kusema haina ubinadamu kwa wafanyakazi wake.
Miongoni mwa masharti yanayoingilia uhuru binafsi wa watu nchini China ni sheria ya familia kuzaa mtoto mmoja tu, sheria iliyowekwa na serikali miaka ya sabini.
Masharti hayo ambayo yamewekwa katika sheria za kampuni hiyo zimezua malalamiko mengi katika mitandao ambapo wanawake wote walio kwenye ndoa lazima wawe wamefanya kazi kwa mwaka mmoja kwenye kampuni hiyo kabla ya kutoa maombi ya kukubaliwa kushika mimba.
Kwa mujibu wa masharti hayo, anayekiuka utaratibu huo na kushika mimba bila ya idhini, atatozwa faini au hapandishwi cheo.
Shirika la utangazaji la China limekosoa vikali kampuni hiyo iliyoko mkoa wa Henan na kusema haina ubinadamu kwa wafanyakazi wake.
Miongoni mwa masharti yanayoingilia uhuru binafsi wa watu nchini China ni sheria ya familia kuzaa mtoto mmoja tu, sheria iliyowekwa na serikali miaka ya sabini.
No comments:
Post a Comment