Wakili Akanusha Kumtesa "House Girl" - LEKULE

Breaking

17 Jun 2015

Wakili Akanusha Kumtesa "House Girl"

WAKILI wa kujitegemea Yasinter Rechungura (45), ametoa ushahidi Mahakamani na kudai kwamba aliyekuwa mfanyakazi wake wa ndani Merina Mathayo (16), hakuwahi kumpiga wala kumjeruhi badala yake  alijeruhiwa wakati akichota maji katika SIMTANK lililopo nyumbani kwake Boko Magengani.
 
Yasinter alitoa ushahidi huo jana Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni Dar es Salaam mbele ya Hakimu Amalia Mushi, na Upande wa Jamhuri ukiongozwa na Masini Musa wakati  Wakili wa utetezi Benitho Mandele.
 
Alidai kuwa Merina siku moja wakiwa nyumbani Merina alienda kuchota maji katika simtank lililopo kando ya nyumba ndipo aliteleza na kuanguka juu ya sehemu iliyokuwa na vigae, mawe, mbao, matofali na kuumia kichwani na sehemu nyingine.
 
Mheshimiwa mimi mwenyewe nilishangaa kama mzazi kwa kuwa Merina baada ya kurudi kuchota maji alikuwa anavuja damu nyingi sehemu za usomi ila baada ya kumwuliza hakunipa jibu sahihi ili nilihisi alianguka kwenye hilo tanki la maji kwa kuwa nilipokuwa ndani nilisikia kishindo.
 
“Baada ya kuona hali ile kwanza nilichanganyikiwa kisha nikawapigia simu wadogo zangu Flora na Josephine waje wanisaidie kumpeleka Hospitali kwani mimi nilikuwa nina mtoto mdogo ambaye naye hali yake ki afya haikuwa njema,” alidai Yasinter.
 
Awali aliiambia Mahakama hiyo kwamba Merina alipokuja nyumbani kwake kutoka Bukoba alikuwa anaonekana akiwa na alama za makovu kichwani kwake na baada ya siku kadhaa alipomwuliza alimwambia kwamba yalisababishwa na kupigwa na baba yake wakati mengine aliumia akicheza na wenzake.
 
Aidha, kwa maelezo hayo wakili huyo aliiomba mahakama iangalie suala hilo kwa kina kisha imfutie shauri hilo na kumwachia huru kwani hakutenda kosa hilo kwa kuwa yeye pia ni mzazi mwenye watoto kama Merina.
 
Shahidi wa pili wa utetezi  Josephine Rwechungura (48), alidai kuwa wakati akiendelea kumtibu Merina  katika Hospitali ya Mwananyamala alishangaa umati wa watu ukimvamia na kuanza kumhoji kwamba ni kwa nini anataka kuua mtoto?
 
“Mheshimiwa nikiwa Haspitali ya Mwnanyamala walikuwa Waandishi wa habari, Wanaharakati, watu kutoka Kituo cha Sheria na haki za binadamu LHRC pamoja na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), wakiwa na polisi wakaanza kuni hoji.
 
“Niliambiwa kuwa mimi ni mtesaji, muuaji kitu ambacho ni uongo kwa kweli niliishiwa nguvu kwani nilikuwa namletea mgonjwa chakula,” alidai Josephine.
 

Alilaani kitendo cha askari wa kituo cha Polisi Kawe baada ya kumkamata alilazimishwa kutia saini maelezo ambayo tayari yalikuwa yameandikwa bila kupewa muda wa kuyasoma wala kusomewa kosa lake.

No comments: