ANKO ANASWA GESTI NA MTOTO WA DADAKE - LEKULE

Breaking

22 Jun 2015

ANKO ANASWA GESTI NA MTOTO WA DADAKE

Tap! Jamaa mmoja, mkazi wa Gongo la Mboto-Mzambarauni jijini Dar ambaye jina lake halikufahamika amewekewa mtego wa nguvu kisha kunaswa akiwa katika harakati za kutaka kujivinjari na binti wa miaka 14, ambaye ni mtoto wa dada yake wa tumbo moja (jina linahifadhiwa).

MCHAPO KAMILI

Kwa mujibu wa chanzo chetu, tukio hilo lilijiri hivi karibuni ambapo ‘anko’ huyo ambaye ni dereva wa magari ya benki maarufu jijini Dar, alidaiwa kumsumbua binti huyo wa sekondari kwa muda mrefu.
Ilisemekana kwamba, kwa mujibu wa binti huyo, anko wake alikuwa akimnunulia soda baridi na kumuahidi kuendelea kumfanyia hivyo endapo atakubali ombi lake.

lidaiwa kwamba, baada ya kuona usumbufu umezidi, binti huyo aliamua kukisanua kwa mzazi wake ndipo mtego bab’kubwa’ ukawekwa.

 MAKUTANO GESTI

Baada ya mzazi kumpa mbinu zote za kuhakikisha hajirahisishi kwa mjomba wake, alitakiwa kumseti ili aumbuke ndipo binti akakubaliana na mjomba huyo wakutane gesti (jina kapuni) iliyopo maeneo hayo ya Mzambarauni.

KIBANO

Kwa mujibu wa shuhuda wetu, mjomba mtu akiwa anajiandaa ‘kumtoa kafara’ mtoto wa dada yake ndipo dada mtu na shemeji yake wakaibukia gesti chumba namba 02 na kuzua timbwili la kukata na mundu kwa kumtia mtuhumiwa mikononi kwa msaada wa polisi.
Baada ya kutiwa mikononi na baba wa mtoto wa kike, aliamua kumpeleka hadi kwa askari mmoja anayelinda benki na kumpaki gari kwa lengo la kumpeleka mtuhumiwa kwenye kituo kidogo cha polisi kilichopo maeneo hayo ya Mzambarauni.
Hadi ‘shushushu’ wetu anaondoka kituoni hapo, jamaa huyo alikuwa akihojiwa huku akiomba suala hilo wakalimalize nyumbani.

No comments: