AI:Polisi wanakiuka haki Nigeria - LEKULE

Breaking

5 Jun 2015

AI:Polisi wanakiuka haki Nigeria


Afisa wa ngazi ya juu katika kitengo kinachohusiana na haki za kibinadamu kwenye shirika la umoja wa mataifa ametoa wito kwa rais mpya wa Nigeria Muhammadu Buhari kufanya hima ili kuanzisha uchunguzi kuhusu madai ya ukiukaji wa haki za kibinadamu unaosemekana ulifanywa na vikosi vya kijeshi vinapokuwa vikipambana na kundi la Boko Haram .

Shirika la kutetea haki za kibinadamu Amnesty International linadai kuwa zaidi ya watu elfu 8 walifariki wakiwa katika vizuizi vya maafisa salama.

Afisa huyo wa umoja wa mataifa , Zeid Ra'ad Al-Hussein, ameshtumu ukatili unaofanywa na kundi hilo la Boko Haram dhidi ya raia wasio na hatia.

Serikali ya Nigerian imesema zaidi ya watu 30 wameuawa katika shambulio la hapo jana linaloshukiwa limefanywa na wapiganaji hao wa Boko Haram ambao wamehusika katika mashambulio mengine mengi yaliyosababisha maafa kama hayo.


No comments: