Mchezaji kugharamia hasara ya bao lake - LEKULE

Breaking

11 May 2015

Mchezaji kugharamia hasara ya bao lake


Mchezaji kandanda ameahidi kulipia hasara iliyosababishwa na shabiki wake alipofunga bao.

Shabiki huyo sugu Ross Morgan, 25, alikuwa akitizama mechi kati ya Ipswich na Norwich jumamosi iliyopita wakati huo timu yake ikiwa nyuma kwa bao moja.

Hata hivyo anasema alishikwa na wazimu akaruka juu na kupiga ngumi dari ya nyumba yake ikatoboka baada ya Paul Anderson kufunga bao la kusawazisha.

Morgan aliipiga picha shimo hilo na akaiweka kwenye mtandao wake wa kijamii wa Twitter.

Mashabiki wenza waliisambaza na ikamfikia Anderson ambaye ilimgusa na akajitolea kugharamia hasara aliyosababisha.

No comments: