IS yashambuliwa Iraq,kiongozi mkuu auawa - LEKULE

Breaking

14 May 2015

IS yashambuliwa Iraq,kiongozi mkuu auawa

Waziri wa ulinzi wa Iraqi amesema kwamba kiongozi wa pili wa ngazi ya juu katika mamlaka za kundi la wanamgambo wa dola ya kiislamu IS, ameuawa katika mashambulio ya anga na majeshi ya Marekani kwa kushirikiana na majeshi washirika.
Msemaji wa wizara ya ulinzi wan chi hiyo, ameiambia BBC kuwa Abu Alaa al-Afari aliuawa pamoja na seti kadhaa za wanamgamboa wa dola hiyo katika eneo la Tal Afar lililoko kaskazini mwa nchi hiyo ya Iraq.
Lakini waziri wa mambo ya ndani wa Iraq ametilia shaka juu ya kauli hiyo,nayo Marekani haijathibitisha juu ya kauli hiyo mpaka sasa.
Inaaminika kwamba Al-Afari alichukua madaraka ya kuwa kiongozi mkuu wa kundi hilo la is wiki kadhaa baada ya kiongozi wao mkuu, Abu Bakr al-Baghdadi,kupata majeraha makubwa baada ya kushambuliwa kutokea angani .

No comments: