IS latoa ukanda wa video wa Al Baghdad - LEKULE

Breaking

15 May 2015

IS latoa ukanda wa video wa Al Baghdad


Kundi la Islamic State limetoa ujumbe kupitia mkanda wa video ambao linasema ulinaswa na kiongozi wake, Abu Bakr al-Baghdadi.

Hakujakuwa na uthibitisho wa hakika lakini wachambuzi wanasema kuwa sauti hiyo inafanana na yake.

Al-Baghdadi inasemekana alijeruhiwa vibaya mwezi Machi.

Lakini mwandishi wa BBC anasema kuwa sauti hiyo haifanani ya mtu aliyedhohofika kiafya.

Ujumbe huo unazungumzia mashambulizi yaliyotekelezwa na jeshi la Saudia huko Yemen kuanzia machi ishirini na sita kumaanisha kuwa huenda kanda hiyo haijazidi wiki saba tangu irikodiwe.

No comments: