Mtoto azaliwa bila pua - LEKULE

Breaking

7 Apr 2015

Mtoto azaliwa bila pua



Eli Thompson alizaliwa tarahe nne Machi jioni, lakini alikuwa na kasoro moja, hakuwa na pua.

Siku niliyojifungua, kila kitu kilikuwa sawa.'' Mamake Brandi McGlathery ameambia ABC News Today nchini Marekani.

''Alipozaliwa daktari alimweka kifuani mwangu. Nilipomwangalia kwa karibu, nilisema ' Hana pua'. Walimchukua na kutoka naye.

McGlathery amesema kwamba daktari alikaa kando ya kitanda chake ili kumweleza hali ya mtoto wake. ''Alikuwa amehuzunika..''Amesema.'' Nilijua papo hapo kuwa hakuwa sawa.''

Hata ingawa mtoto wake hakuonyesha kasoro zozote zaidi, McGlathery amesema kuwa alishangazwa na kuhuzunika kutokana na habari hizo.

Lakini licha ya kukosa pua, Brown amesema kuwa mtoto huyu ana afya nzuri na pia ni mtoto mrembo.

No comments: