Man United yaisakama Mancity 4-1 - LEKULE

Breaking

12 Apr 2015

Man United yaisakama Mancity 4-1


Manchester United ilipanda tena katika nafasi ya tatu katika jedwali la ligi ya Uingereza ikiwa pointi moja nyuma ya Arsenal baada ya kuwacharaza mahasimu wao wa jadi Manchester City mabao 4-2.

Sergio Aguerro alikuwa wa kwanza kuiweka City kifua mbele lakini vijana wa Old Trafford walisawazisha kupitia Ashley Young .

Maruane Fellaini alifunga kichwa kizuri kilichoiweka Manchester United kifua mbele kabla ya kiungo wa kati Juan Mata kufunga bao zuri.

Chris Smalling alipiga kichwa kisafi kilichomwacha kipa wa City bila jibu kabla ya Aguero kufunga bao la kufutia machozi na la pili kwa upande wa City ambo kwa sasa wamepoteza mechi sita kati ya nane walizocheza.

Katika mechi ya mapema viongozi wa ligi Chelsea waliendelea na matokeo mazuri baada ya kuwachapa wenyeji wao QPR bao 1-0.

Kiungo wa kati wa Chelsea Cesc Fabregas ndiye aliyefunga bao hilo la pekee.

No comments: