Zitto Kabwe Achaguliwa Kuwa Mkuu wa Chama cha ACT-Tanzania - LEKULE

Breaking

30 Mar 2015

Zitto Kabwe Achaguliwa Kuwa Mkuu wa Chama cha ACT-Tanzania


Kiongozi mpya wa chama cha ACT Tanzania, Zitto Kabwe akionyesha alama ya chama ambayo ni "Uwazi" baada ya kuchaguliwa.

Zitto Kabwe, akilakiwa na wajumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho, wakati wa uchaguzi mkuu uliofanyika kwenye ukumbi wa Kadinali Rugambwa, Oysterbay jijini Dar es Salaam, Jumamosi Machi 28, 2015.

Zitto alichaguliwa kuwa kiongozi wa chama hicho nafasi ambayo kwa katiba ya chama hicho ndiyo ya juu zaidi.

Nafasi zingine ni Mwenyekiti wa chama, na makamu wake, wa Tanzania visiwani na Tanzania bara, hali kadhalika nafasi ya ukatibu mkuu na manaibu wake wiwili.
Mama Anna Mughwira kawa Mwenyekiti wa kwanza wa chama cha ACT Wazalendo na kuweka rekodi nchini Tanzania ya kuwa Mwenyekiti wa Taifa mwanamke.

Wajumbe wa NEC wa ACT Wazalendo waliochaguliwa:

Zanzibar
Halima M Hamis
Said Ismail
Rashid S Ali
Juma Said Saanane
Halua Ali Amali

Tanzania Bara
Marunga Msimba
Ali Mwinyi
Sophia Yamola
Fungo G Benson
Charles Lubala
Godfrey Sanga
Likapo B Likapo
Batulo Ibrahim
Kirungi A Kirungi
Alex Nsanga

Chama hicho kitazinduliwa rasmi leo Jumapili kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

No comments: