Shirikisho la mbio za Biaskeli lawamani - LEKULE

Breaking

9 Mar 2015

Shirikisho la mbio za Biaskeli lawamani



Shirikisho la Mbio za baiskeli duniani limelaumiwa kwa kufumbia macho tatizo la kutumia dawa zilizopigwa marufuku za kusisimua misuli michezoni.

Baada ya mwaka mmoja wa uchunguzi ulifanywa na tume iliyoundwa imesema katika miaka ya 1990 katika karne hii shirikisho hilo lilifumbia macho marufuku ya kutumia dawa za kusisimua misuli.

Shirikisho hilo limetupiwa lawama kuwa lilishindwa kutumia kanuni zake ipasavyo. Pia limelaumiwa jinsi lilivyoshughulikia suala la mwendesha baiskeli raia wa Marekani Lance Armstrong kwa madai kwamba alipewa upendeleo japo baadae alifungiwa moja kwa moja kushiriki michuano ya baiskeli

No comments: