MH. LUKUVI AANZA ZIARA MKOANI RUKWA - LEKULE

Breaking

27 Mar 2015

MH. LUKUVI AANZA ZIARA MKOANI RUKWA


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Injinia Stella Manyanya alipowasili uwanja wa ndege wa Sumbawanga kuanza ziara ya kutatua migogoro ya ardhi Mkoani humo.

Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu akimpokea Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi alipowasili eneo la Jangwani mjini Sumbawanga kuweka jiwe la msingi katika nyumba za makazi zinazojengwa na NHC kwa ajili ya kuuzia wananchi.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akisalimiana na Kamishna msaidizi wa ardhi kanda ya nyanda za juu kusini Bw. Msigwa mara alipowasili Mkoani Rukwa kutatua migogoro ya ardhi.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akitoa msimamo wa dhati wa serikali (kwa wananchi waliofurika kumsikiliza hawapo pichani) wenye nia ya kutatua mgogoro wa ardhi uliopo kati ya mwekezaji na wananchi wa vijiji vya Skaungu na Mawensuzi alipofika katika eneo la Malonje Wilayani Sumbawanga.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akihutubia halaiki ya wananchi waliohudhuria sherehe za uwekaji jiwe la msingi kwenye nyumba za makazi zinazojengwa na NHC eneo la Jangwani Mkoani Rukwa. Alisisitiza Halmashauri nchini kutenga ardhi kwa ajili ya NHC kujenga nyumba za gharama nafuu.

Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu akitoa maelezo ya mradi wa nyumba za makazi zinazojengwa na NHC eneo la Jangwani mjini Sumbawanga kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi (hayupo pichani) jana.

Mbunge wa Sumbawanga Mhe. Hilal Aeshi akiishukuru NHC kwa kujenga nyumba za makazi eneo la Jangwani kwa ajili ya kuuzia wananchi.

Mwenyekiti wa kijiji cha Skaungu Bw. Pascal Mwanakatwe akisoma risala kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi kuelezea mgogoro wa ardhi unaokabili kijiji hicho na mwekezaji kanisa la Efatha baada ya Waziri Lukuvi kufika eneo la Malonje kuwasikiliza wananchi ili serikali ipate mwelekeo wa kutatua mgogoro huo.


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akisikiliza na kupokea barua za malalamiko ya wananchi waliofurika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa jana ili kuwasilisha kero zao za ardhi.

No comments: